» » Misaada ya chakula haiwafikii walengwa

Nigeria

Image captionYemi Osinbajo mwenye kofia nyeusi akiwa pamoja na Kashim Shettima
Maofisa nchini Nigeria wamearifu kwamba nusu ya chakula cha msaada kilichokuwa kimepelekwa kwa watu waliosambaratishwa kutoka katika makaazi yao na kundi la wana mgambo wa kiislam hakijawafikia walengwa.Idadi ya watu hao inakadiriwa kufikia milioni tatu katika kipindi cha miaka nane ya uasi wa wapiganaji wa Boko Haram
Msemaji wa kaimu rais wa Nigeria, Yemi Osinbajo, amesema kwamba mfumo mpya umezinduliwa mapema mwezi huu, na kuleta mabadiliko makubwa katika usambazaji misaada ya kibinaadamu, huku dhana ya kuibwa kwa misaada hiyo na kwenda katika mikono isiyostahili ikirindima.
Kwa sasa, maelfu ya polisi na wanajeshi wamechukua hatua ya kusindikiza magari hayo yenye kusambaza misaada ya chakula, ili iweze kufika katika maeneo stahiki na kuwapa wenye uhitaji.
Zaidi ya magari ya misaada milioni moja yaliyosheheni nafaka yako njiani kuelekea Kaskazini Magharibi mwa nchi hiyo. Watu milioni moja unusu wako katika njaa kuu.
Nao wapiganaji wa Boko Haram wanaendelea na mashambulizi bila kukoma, pamoja na mashambulizi na wakati mgumu wanaokabiliana nao kutoka katika jeshi la Nigeria.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...