» » China inataka kuwa nchi ya mfano katika kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi

China

Image captionMabadiliko ya tabia nchi
China imeahidi kutekeleza majukumu yake katika makubaliano yaliyowekwa ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi licha ya kuwa Marekani haitoshiriki katika makubaliano hayo.
Akizungumza nchini Ujerumani waziri mkuu wa China, Li Keqiang amesema inapenda kukabiliana na suala la mabadiliko ya tabia nchi.
Na kuongeza kuwa, nchi yake, inataka kuwa nchi ya kupigiwa mfano katika harakati za kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
Kwa upande wake, rais wa Marekani Donald Trump anatarajiwa kutangaza maamuzi yake kuhusiana na makubaliano ya Paris ya mwaka 2015 hapo baadae, huku baadhi ya taarifa kutoka nchini Marekani
zinasema kuwa rais Trump atajiondoa katika mkataba huo.
China
Image captionWaziri Li Keqiang
"China itaendea kutekeleza makubaliano yaliyofanywa katika mkutano wa Paris lakini pia tunatarajia kuyafanya haya kwa kushirikiana na nchi nyingine," alisema waziri Li.
China ikiwa miongoni mwa mataifa makubwa ambayo imeamua kutekeleza majukumu yake katika kujaribu kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.
China
Image captionLi Keqiang amesema inapenda kukabiliana na suala la mabadiliko ya tabia nchi.
Urusi pia imesema itaendelea kubaki katika wajibu wake kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa lakini wamesema kuwa makubaliano hayo yatapata pigo iwapo Marekani itajitoa.
"Tunaendelea bila kusema kwamba ufanisi wa mazungumzo haya utakuwa umepoteza nguvu kwa kukosekana kwa washiriki wake wakuu," amesema Kremlin.
Kwa sasa waziri wa mambo ya ndani wa Uingereza Boris Johnson amesema alikuwa na shauku kuhusiana na uamuzi wa Marekani kujiondoa na kuongeza kwamba anaamini rais Trump angelitafakari suala hilo kwa namna ya pekee.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...