Shirika la Afya Duniani, WHO limeahidi kuchukua hatua za tahadhari na haraka za haraka, ili kuzima mlipuko wa ugonjwa hatari wa Ebola kaskazini mwa Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Inasema kuwa wataalamu wake wa kiufundi, wametumwa hadi maeneo ya vijijini, kunako aminika kutokea visa 11 vya ugonjwa wa Ebola -- zikiwemo ripoti ya vifo vya watu watatu.
- Ugonjwa wa Ebola waripotiwa DR Congo
- Chanjo ya Ebola yafanikiwa
- Guinea: Wanawake wajawazito hukwepa hospitali wakihofia Ebola
Wanafanya kila mbinu kubaini upana wa mlipuko wa ugonjwa huo, kuwapa tiba walioambukizwa na virusi vya ugonjwa huo, na kuwatambua walioambukizwa au watu waliokaribiana na walioambukizwa virusi hivyo.
Huu ni mlipuko wa 8 uliotambuliwa wa Ebola nchini Congo, tangu kisa cha kwanza kutambuliwa cha Ebola nchini humo mnamo mwaka wa 1976.
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440
BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI
No comments:
Post a Comment