» » Venezuela: Maandamano yaendelea

Maduru
Image captionwaandamanaji Venezuela kufunga barabara
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro amekosolewa ndani na nje ya nchi yake kuhusu mpango wa kuunda bunge litakaloandika katiba mpya.
Katibu mkuu wa jumuia ya nchi za Amerika, OAS, Luiz Almagro amesema hatua hiyo haikubaliki na ni kinyume cha katiba.
Marekani imesema kuwa bunge la katiba ni njama tu za kumfanya Maduro aendelee kubaki madarakani huku Brazil nayo ikisema kuwa huo ni mpango wa kufanya mapinduzi.
Bunge la Congress linalodhibitiwa na upinzani limepiga kura kukataa bunge jipya la katiba, likisema kuwa halitaundwa bila wao kuridhia.
Venezuela
Image captionMaandamano kupinga katiba mpya,Venezuela
Wakati hayo yakijiri, katika hatua nyingine waandamanaji kwa mara nyingine wamejitokeza barabarani na kusababisha misururu mirefu ya magari.
Wakati rais Maduro akiona kwamba hatua hii ni ya kuwavunja nguvu wapinzani ambao amewashutumu kutaka kumpindua, hasimu wake Henrique Capriles amesema hayo ni maneno ya serikali iliyoshindwa ambayo inataka kukwepa kuitisha uchaguzi.
Amesema maandamano yataendelea.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles