» » Marekani: Tutaisambaratisha Korea Kaskazini tukilazimishwa

Rais wa Marekani, Donald Trump amezionya nchi za Korea ya Kaskazini na Iran kufuatia vitisho vinavyotolewa na nchi hizo vya kufanya majaribio mbalimbali ya silaha za nyuklia, huku akisema kuwa atazigeuza mavumbi kama ikibidi.

Ameyasema hayo katika hotuba yake aliyoitoa katika mkutano wa Baraza la Umoja wa Mataifa unaoendelea Jijini New York, ambapo amesema kuwa silaha za nyuklia ni tishio kwa usalama wa dunia.

Aidha, Katika hotuba yake hiyo ya kwanza katika mkutano wa Baraza la Umoja huo unaofanyika Jijini New York, Trump ameonya kuwa Marekani itaiangamiza Korea kaskazini iwapo italazimika kujitetea ama kuwalinda washirika wake.

Hata hivyo, katika hatua nyingine Trump amesema kuwa Iran ni nchi ya kifisadi inayoongozwa kidikteta, hivyo ameitaka kuacha mara moja kusaidia makundi ya kigaidi ambayo yamekuwa yakihatarisha amani ya mashariki ya kati.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...