» » Trump amtetea mkwe wake Jared Kushner kuhusu Urusi


Jared Kushner na Donald Trump

Haki miliki ya pichaREUTERS
Image captionJared Kushner ni mmoja wa wasaidizi wakuu wa Donald Trump
Rais wa Marekani Donald Trump amejitokeza kumtetea mkwe wake Jared Kushner, baada ya taarifa kutokea kwamba Kushner, ambaye kwa sasa ni mshauri wake katika ikulu ya White House, alijaribu kuanzisha njia ya kisiri ya mawasiliano na maafisa wa Urusi.
Kwenye taarifa ambayo imekabidhiwa gazeti la New York Times, Bw Trump amemsifu Kushner na kusema kwamba anafanya "kazi nzuri".
Hata hivyo, hajazungumzia moja kwa moja tuhuma zinazomkabili mwanamume huyo ambaye ni mumewe binti wa kwanza wa Bw Trump, Ivanka.
Taarifa zinadai kwamba Bw Kushner alijadiliana na balozi wa Urusi kuhusu uwezekano wa kuanzisha njia ya kisiri ya kuwasiliana na maafisa wa Urusi mwezi Desemba.
Magazeti ya New York Times na Washington Post yanasema alitaka kutumia huduma za Urusi kukwepa mawasiliano hayo kusikika na majasusi ya Marekania akiwasiliana na maafisa wa Moscow.
Anadaiwa kufanya hivyo kabla ya Bw Trump kuapishwa kuwa rais, na kwa hivyo wakati huo alikuwa tu raia wa kawaida.
Tuhuma hizo zimeibuka baada ya Bw Kushner kudaiwa kuwa miongoni mwa wanaochunguzwa na FBI kuhusu tuhuma kwamba Urusi iliingilia uchaguzi wa Marekani mwaka 2016.
Taarifa nchini Marekani zinasema maafisa wana habari muhimu, lakini kwamba si lazima iwe kwamba hilo lilikuwa kosa la jinai.
Ivanka Trump na Jared Kushner Mei 23, 2017Haki miliki ya pichaAFP
Image captionKushner ni mumewe binti wa kwanza wa Trump, Ivanka
Bw Trump, ambaye inadaiwa alikutana na mawakili White House siku ya Jumapili, ambaye bado anamuunga mkono Bw Kushner, ambaye kwa sasa ni mshauri wa ngazi ya juu White House.
"Jared anafanyia nchi hii kazi nzuri sana. Nina imani naye kikamilifu," alisema kupitia taarifa kwa New York Times.
"Anaheshimiwa na karibu kila mtu na anafanyia kazi mipango ambayo itasaidia nchi yetu kuokoa mabilioni ya dola. Kadhalika, na labda muhimu zaidi, yeye ni mtu mwema."
Matamshi ya Bw Trump yametokea baada ya maafisa wakuu wa utawala wake kupuuzilia mbali tuhuma hizo, bila kusema iwapo zilikuwa za kweli.
Waziri wa usalama wa ndani John Kelly aliambia ABC News Jumapili kwamba ni kawaida kuwa na njia za kisiri za kuwasiliana na mataifa yenye ushawishi.
Mshauri wa usalama wa taifa wa Bw Trump HR McMaster pia alisema "tuna njia za faragha za kuwasiliana na mataifa kadha."

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...