» » Rais Magufuli: Napata Machungu na Majonzi Ninapoyaona Haya Majeneza ya Watoto Wetu

Rais Dkt Magufuli ameshindwa kujizuia na kusema kuwa amekumbwa na majonzi makubwa baada ya kuona majeneza 35 ya wanafunzi wa Shule ya Lucky Vicent ya jijini Arusha waliofariki katika ajali ya basi wilayani Karatu Mkoani Arusha.

Rais Magufuli ameyasema hayo wakati miili ya wanafunzi 35, walimu 2 na dereva mmoja ikiagwa katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha na kisha kusafirishwa maeneo mbalimbali kwa ajili ya maziko.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Dkt Magufuli aliandika, “Nimepatwa na uchungu na majonzi makubwa ninapoyaona majeneza ya watoto na walezi wao waliopoteza maisha katika ajali ya basi huko Arusha .”

“Tumewapoteza mashujaa wetu ktk elimu. Tuwaombee na tuendelee kuwa na subira, uvumilivu na ustahimilivu 2/2.”

Aidha, Rais Dkt Magufuli amewasihi wa Tanzania kuendelea kuwa wamoja wakati wakiomboleza tukio hili kubwa lililoikumba nchi na kuacha simanzi miongoni mwa watu wengi.

“Tunapoomboleza vifo vya wapendwa wetu tuendelee kuwa wamoja. Mungu ibariki Tanzania.”

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...