» » ONYO kwa Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi Jijini Mwanza

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella amewazuia wakuu wa wilaya na wakurugenzi wa halmashauri zote mkoani humo kutoka nje ya vituo vyao vya kazi hadi watakapofikia lengo la kukusanya asilimia mia ya mapato ya ndani kabla au ifikapo Juni 30, mwaka huu.

Akihutubia mkutano wa mwaka wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa (Alat), Mkoa wa Mwanza mjini Nansio, Ukerewe leo , Mongella ameonya kuwa wakuu wa wilaya na wakurugenzi ambao halmashauri zao zitashindwa kufikia malengo watakuwa wamepoteza sifa za kuendelea kushika nyadhifa zao.

"Hata wenyeviti na mameya ambao halmashauri zao zitakusanya chini ya asilimia mia watasalia kwenye nafasi zao kwa sababu tu wamechaguliwa kwa kura, lakini watakuwa wamedhihirisha udhaifu wao katika usimamizi," amesema Mongella

Amesema hadi kufikia robo tatu ya mwaka wa fedha 2016/17, halmashauri zote nane za Mkoa wa Mwanza zilikusanya mapato kwa asilimia 51 pekee.

"Asilimia 49 iliyosalia lazima zikusanywe ifikapo Juni 30, mwaka huu. Namna mtakavyofanya mimi sijui. Lakini tusije tukaelewana vibaya muda huo ukifika bila makusanyo kufikia asilimia mia moja."

Mkoa wa Mwanza una wilaya saba za Ilemela, Nyamagana, Ukerewe, Kwimba, Magu, Sengerema na Misungwi zenye halmashauri nane.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles