» » Wanafunzi Vyuoni wapata somo kwa TCRA



Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA), imewataka wanafunzi wa vyuo vikuu nchini na wananchi kutumia huduma za mawasiliano kwa faida, badala ya kuzitumia kujiburudisha pekee.

 

Mhandisi wa Masafa wa TCRA, Francis Mihayo alisema hayo hivi karibuni wakati wa kongamano la vyuo vikuu kujadili matumizi sahihi ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (Tehama), lililofanyika katika Chuo Kikuu cha Tumaini Makumira mkoani Arusha. Mihayo alisema kumekuwa na matumizi yasiyo sahihi ya mitandao hasa kwa wanafunzi wa vyuo vikuu, ambao baadhi wameingia matatani kutokana na kuTOzingatia sheria.

 

Waziri wa Habari na Mawasiliano wa Serikali ya Wanafunzi wa chuo hicho, John Semindu alisema wameamua kuandaa kongamano hilo ili kutoa nafasi kwa wanafunzi kujifunza matumizi sahihi ya na kujiepusha kusambaza ujumbe wenye lengo la kusababisha uvunjifu wa sheria. 

Semindu alisema kutokana na kukua kwa huduma za mawasiliano nchini na duniani, ni watu wachache wanaotumia huduma hizo zaidi ya kuwasiliana.

 

“Tunatakiwa twende mbali zaidi ya kuwasiliana na kutumiana ujumbe kutufanya tucheke, bali tunaweza kutumia huduma za Tehama kujiajiri na kuajiri wengine ni eneo muhimu katika kurahisisha kazi na kuchochea ubunifu ambao ndiyo msingi wa maendeleo,” alisema Semindu.

 

Richard Gwele, kutoka Taasisi ya Smart Education na Mwangaza Jafar ambaye ni mwanafunzi wa Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru, walisema elimu zaidi inapaswa kutolewa ili kuepusha matumizi yasiyo sahihi hasa kwenye mitandao ya jamii.

 

Gwele alisema iwapo wanafunzi watatumia mitandao vizuri itawasaidia kupata kujisomea mambo mbalimbali hasa yanayotokana na mabadiliko ya teknolojia duniani.

 

Alisema wanafunzi hawajatumia hata nusu ya mitandao katika kujielimisha, hivyo wanatakiwa kubadilika.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...