» » Trump kulaani shambulio la kemikali yenye sumu,Syria

Trump kulaani shambulio la kemikali yenye sumu,Syria

syriaHaki miliki ya pichaGOOGLE
Image captionRais wa Marekani Donald Trump
Rais wa Marekani Donald Trump amelielezea shambulio la kuhusisha gesi yenye kemikali zenye sumu dhidi ya watu wakati wa mashambulizi ya anga kaskazini mwa Syria kuwa ni tukio lisilo la kibinaadamu.
Marekani na mataifa mengine ya magharibi yamemshutumu Rais wa Syria, Bashar Assad na serikali yake kwa kile walichodai shambulio la kutumia silaha za kemikali la siku ya jumanne mjini Khan Sheikhoun.
Trump amesema vifo vya watoto vimebadili mtazamo wake kwa Assad.
syriaHaki miliki ya pichaAFP
Image captionmtoto aliyeathirika katika shambulio la kemikali
''na nitakueleza, kuwa shambulio lile dhidi ya watoto limenifanya niwe na mtazamo mwingine. Ni kitu cha kutisha inatisha sana, na nimekuwa nikifuatilia na kutazama, hakuna namna nyingine zaidi naweza kusema, imekwishatokea kuwa sasa mtazamo wangu kwa Syria na Assad umebadilika sana.''
Marekani, Uingereza na Ufaransa, zote zimemshutumu mshirika wa Serikali ya Syria kwa kile kilichotoka katika mji wa Khan Sheikhoun.
Waziri wa mambo ya nje wa Marekani, Rex Tillerson ambaye anatarajiwa kufanya ziara mjini Moscow nchini Urusi juma lijalo, ameitaka Urusi ifikiri kwa makini kuhusu uhusiano wake na Syria
syria
Image captionShambulio la kemikali,Syria
hakuna shaka yeyote kuwa utawala wa Syria chini ya Bashar Al Assad unahusika na shambulio hili la kinyama na tunaona sasa ni wasaa kwa warusi kufikiri kwa makinni kwelikweli kuhusu kuendelea kuunga mkono utawala wa Assad''
Urusi imepinga msimamo wa marekani na mataifa ya magharibi kuhusu tukio hilo na kusema kuwa , mswada kuhusu azimio la baraza la usalama la umoja wa mataifa kuhusu shambulio hilo ni chuki dhidi ya Syria.
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en





tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles