» » Trump amshutumu Bashar Al Assad kama mtu katili

Trump amshutumu Bashar Al Assad kama mtu katili

Rais wa Syria Bashar Al AssadHaki miliki ya pichaAFP
Image captionRais wa Syria Bashar Al Assad
Rais wa Marekani Donald Trump amemshutumu Rais Bashar Al Assad kama mtu katili na pia ametaka kumalizwa kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Syria.
Akizungumza katika mkutano wa pamoja wa waandishi wa habari, akiwa pamoja na Katibu mkuu wa Jumuia ya Kujihami ya Nchi za Magharibi -NATO- Jens Stoltenberg, Rais Trump amelaani kile alichokiita mauaji ya kikatili ya raia wasio na hatia katika shambulio la wiki iliyopita, ambalo linadaiwa kutumia silaha za kikemikali katika mji unaoshikiliwa na waasi wa Khan Sheikhoun.
Akiielezea Urusi kuwajibika kwake katika shambulio hilo, Rais huyo wa Marekani amesema ni jambo la kusikitisha.
Rais Trump amesema hana shaka yoyote kwa sababu amefanya jambo lililo sahihi kutoa agizo la kushambuliwa kwa makombora katika kambi ya jeshi la anga ya Shayrat nchini Syria.
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en


tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles