» » Roma Afunguka Haya kwa Uchungu Mara Baada ya Kupatikana Jana Usiku

Inasikitisha..Roma Afunguka Haya kwa Uchungu Mara Baada ya Kupatikana Jana Usiku...!!!!


Hatimaye msanii Roma Mkatoliki akiwa na wenzake watatu amezungumza na vyombo vya habari kwa mara ya kwanza kufuatia tukio la kutekwa na watu wasiojulikana kwa takribani siku tatu.

Roma na wenzake wamejitokeza mbele ya vyombo vya habari baada ya kutoka katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam, walikoenda kupimwa afya zao baada ya kuhojiwa kwa takribani saa sita katika kituo cha polisi cha Oysterbay.

Msanii huyo amewashukuru watanzania kwa ushirikiano wao waliouonesha na kuwahakikishia kuwa wako salama kiafya. Alisema ingawa hajaingia kwenye mitandao lakini ameelezwa juhudi zilizofanywa na watanzania.

“Niwahakikishie mimi ni mzima kabisa mpaka sasa hivi, niko salama kiafya na hata kiakili. Na hata wenzangu watatu, Moni, Laden na Imma… niwahakikishie kabisa kuwa sisi wote ni wazima na tunaendelea vizuri,” alisema Roma na kuomba wapewe nafasi kwanza wakapumzike.

Aliongeza kuwa kwa sasa wako katika taratibu za kuelezea vyombo vya usalama kuhusu tukio zima la kutekwa kwao hivyo hawawezi kuweka wazi kwa umma kwa sasa.

Aidha, Roma ameahidi kuwa siku ya Jumatatu watazungumza na vyombo vya habari na kuueleza umma kuhusu undani wa kilichojili.

Roma na wenzake walitekwa na watu wasiojulikana katika studio za Tongwe Records ambapo watu hao walichukua pia vifaa vya studio hiyo ikiwa ni pamoja na ‘computer’ na runinga bapa, kwa mujibu wa mmiliki wa studio hizo.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en

tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles