» » Rais Maduro: venezuela aomba mazungumzo na upinzani

Rais Maduro wa venezuela aomba mazungumzo na upinzani

Caracas, 22 April 2107Haki miliki ya pichaAFP
Image captionMaandamano ya karibuni yalifanyika Jumamosi, na kunayo yaliyopangiwa leo Jumatatu
Rais wa Venezuela Nicolas Maduro ameitisha kurejelewa kwa mazungumzo kati ya serikali na upinzani nchini humo.
Kadhalika, amesema kwamba anataka uchaguzi wa majimbo ufanyike.
Amesema hayo baada ya maandamano mengine makubwa kupangwa na upinzani Jumatatu, wiki tatu baada ya maandamano mengine makubwa kutatiza shughuli nchini humo.
Waandamanaji wamekuwa wakitaka uchaguzi mkuu ambao umepangiwa kufanyika mwaka ujao ufanyike mwaka huu na Rais Maduro aachie madaraka.
Mazungumo kati ya upinzani na serikali mwaka jana yalivurugika baada ya upinzani kumtuhumu Bw Maduro kwa kukiuka baadhi ya makubaliano na kutumia mazungumzo hayo kujipatia muda zaidi wa kuendelea kuongoza.
Akihutubu kupitia runinga Jumapili, bw Maduro aliunga mkono pendekezo la kufanyika kwa ucahguzi wa mameya na magavana wa majimbo lakini hakugusia uchaguzi wa urais.
"Uchaguzi - ndio, Ninataka uchaguzi sasa," alisema.
"Hili ndilo ninalosema kama kiongozi wa nchi, kama kiongozi wa serikali."
Uchaguzi wa magavana wa majimbo ulifaa kufanyika Desemba mwaka jana, lakini uchaguzi wa mameya ulifaa kufanyika mwaka huu.
Maandamano makubwa ya upinzani yalifanyika Jumamosi, waandamanaji wakiwa kimya kwa heshima ya watu 20 waliouawa katika maandamano ya karibuni.
Wanaharakati wa kutetea haki za kibinadamu wanasema watu zaidi ya 1,000 walikamatwa wakati wa maandamano hayo na 700 bado wanazuiliwa.
Upinzani unailaumu serikali kwa mgogoro wa kiuchumi ambao umeathiri pakubwa nchi hiyo na kusababisha uhaba wa vyakula, bidhaa muhimu na dawa.
Maandamano yalichocheza na jaribio la Mahakama ya Juu inayodhibitiwa na serikali kutwaa baadhi ya mamlaka ambayo huwa na Bunge.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...