» » Mgomo wa Mabsi na Daladala Wasitishwa

Mgomo wa Mabsi na Daladala Wasitishwa

Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri na Nchi Kavu na Majini, Sumatra, pamoja na wadau wa sekta ya usafirishaji wamekubaliana kusitisha mgomo wa usafirishaji wa abiria na mizigo uliopangwa kuanza kesho.

Akizungumza leo jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe amesema kusitishwa huko kunatokana na kikao na Waziri wa Mawasiliano Uchukuzi na Ujenzi, Prof. Makame Mbarawa, kuhusu kuandika kwa kutenganisha makosa ya dereva na wamiliki wa mabasi

Bw. Ngewe amesema, kanuni hizo zitaandikwa ndani ya siku 14 katika rasimu hiyo na wadau wa usafirishaji kuendelea na shughuli za usafirishaji na kwamba, baada ya kufanya marekebisho ya rasimu ya kanuni itarudishwa kwa wadau kuweza kujadiliwa kwa ajili ya kuwasilishwa Bungeni .

Naye Makamu Mwenyekiti wa Wamiliki wa Mabasi, Taboa, Abdallah Mohamed, amesema wamekubaliana na Sumatra kurekebishwa kwa baadhi ya kanuni za makosa kati ya wamiliki na madereva wa mabasi.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles