mwendelezo wa somo:
Sehemu ya pili
KUSOMAPAMOJANENO LAMUNGU Soma Danieli 1:1-21 1) Kwa nini Danieli na rafiki zake watatu walichaguliwa kupata elimu hiyo? 2) Wakati Danieli na rafiki zake walipochukuliwa mateka, unafikiri walikuwa wanafikiria mambo gani juu ya maisha yao ya usoni? Unafikiri walipenda kuondoka nyumbani na kuishi katika jumba la mfalme? 3) Danieli alichagua kufanya nini katika kipindi hiki cha mafunzo? Mungu aliuheshimu uchaguo wa Danieli na kumtuuza na nini? 4) Kama vile Daniel na rafiki zake walivyokabiliwa na mvuto wa mila, vijana wengi siku hizi wanakabiliwa na mvuto wa mila na jamii kutenda mambo yaliyo kinyume. Baadhi ya mivuto kama hiyo ni ipi? 5) Fikiria juu ya uchaguo ambao Danieli na rafiki zake waliufanya. Unajifunza mambo gani kutoka katika hadithi hii ambayo unaweza kuitumia katika maisha yako? MAMBO YAKUFIKIRIAPAMOJA Kufanya Maamuzi ya Busara Kama vijana hao wanne katika hadithi ya kwanza, pengine nawe pia una ndoto mbali mbali juu ya maisha yako ya usoni. Unaweza kuwa na ndoto ya kuendelea na masomo hadi Chuo Kikuu mara utakapomaliza masomo yako ya shule ya upili. Unaweza kuwa unafikiri juu ya kusafiri katika nchi mbali mbali. Unaweza kuwa na fikira za kuishi nyumbani na kuwa mkulima. Pengine unafikiria juu ya mke utakayemwoa au mme atakayekuoa au vile familia yako itakavyokuwa. Je! Unaweza kutimiza ndoto zako? Wakati mwingine mambo kadhaa yaliyo juu ya uwezo wako yanaweza kukuzuia usitimize ndoto zako. Mara nyingi, ni mambo yale unayoyachagua kila siku yanayoamua ikiwa utatimiza ndoto zako au la. Rafiki ni watu muhimu katika maisha yako. Rafiki unaowachagua ndio watakaokushawishi kutenda na kusema na vile uwezavyo kuutumia wakati wako. Mambo unayoyatenda au kuyasema ndiyo yatakayowafanya watu wengine unaoishi nao wakuheshimu au wakudharau. Vile unavyoutumia muda wako kuyafanikisha masomo yako ama kazi zako nyumbani. Iwapo utafanikiwa shuleni unaweza kuendelea na masomo yako hata kuwa na kazi itakayokupatia mshahara mzuri zaidi kuliko wale ambao hawakuendelea na masomo. Iwapo utafanya kazi kwa bidii shambani utaheshimiwa na wengine katika familia yenu na jumuia yenu. Unaweza kuwa hata kiongozi katika jumuia yako. Uchaguzi mmoja mbaya unaweza kubadilisha mambo kabisa. Ukichagua kuibia mtihani utafukuzwa shuleni.
Ukichagua kufanya mapenzi kabla ya ndoa unaweza kupata UKIMWI kitu ambacho kitakufanya usiishi muda mrefu hadi pale utakapowaona watoto au wajukuu wako. Kufanya uchaguzi si kitu rahisi sana kama vile ambavyo mtu anaweza kufikiria. Wakati mwingine inaonekana kana kwamba kuna mambo mengi ya kuchagua; wakati mwingine kuona kwamba hakuna uchaguo mzuri hata kidogo. Ni mambo gani yanayoweza kukusaidia kufanya uchaguo utakaokusadia utimize ndoto zako? Hizi ni hatua ambazo zinaweza kukusaidia kuamua 1. Orodhesha mambo unayopenda kuchagua Chukua muda kuandika mambo kadhaa unayoweza kuamua kulingana na uamuzi wako utakavyokuwa katika miaka kadhaa ya usoni. Kwa mfano, rafiki yako ameamua kwenda jijini kutafuta kazi na akataka aende pamoja nawe. Mambo gani yaweza kukukabili katika kufanya uamuzi huo? Moja ni kukubali kwenda pamoja na rafiki yako na lingine ni kubaki nyumbani. 1. Fikiria juu ya matokeo mazuri ama mabaya ya kila jambo. Andika matokeo mazuri ama mabaya katika kila uchaguzi ulioandika hapo juu. Kwa mara nyingine tena, yaandike mambo hayo ili uweze kulinganisha kwa urahisi. Je! Kutakuwa na matokeo gani ukienda mjini? Unaweza kupata kazi na kujipatia fedha. Unaweza kuendelea kuishi na rafiki yako atakayekusaidia. Je! Kuna madhara gani yatakayokupata? Utatengana na familia yako. Yawezekana usipate kazi. Utahangaika kupata chakula. 3. Jaribu kufahamu neno la Mungu linavyosema juu ya uamuzi wako Neno la Mungu linatupatia mwongozo wa kila hali inayotukabili. Katika hadithi ya Danieli na rafiki zake tunaona hawakufanya kitu rahisi, lakini pia walifanya kitu sahihi. Mungu aliubariki uchaguo wao mgumu walioufanya. Kutokana na mfano huo, uchaguo sahihi kwako ni upi? 4. Tafuta ushauri wa busara! Chukua muda kuzungumza na watu mbali mbali wanaokufahamu vizuri na unaowathamini kama vile wazazi, shangazi au mjomba, mchungaji, au rafiki yako mzuri juu ya mambo mbali mbali unayoweza kuchagua. Kubali wakuulize maswali kulingana na uamuzi wako. Wanaweza kuwa na mawazo mengine ambayo hukuwa umeyafikiria. 5. Omba Kumbuka kuwa hakuna uamuzi ulio mdogo hata usiweze kuuombea mbele za Mungu (Wafilipi 4:6-7). Usisumbuke iwapo hutapata majibu kulingana na vile ulivyofikiri au kulingana na vile wengine wanavyofanya. Endelea kuleta maswali yako mbele za Mungu naye atakuwa mwaminifu kukujibu kwa njia zake ambao huwezi kutarajia kwa kubadilisha mambo fulani katika maisha, kwa kuubadilisha mtazamo wako ama kwa kuwatumia watu wengine katika maisha yako. Wakati mwingine jibu laweza kuwa "hapana" ama "subiri." Ahadi ya Mungu juu ya maisha yako Ni jambo la kupendeza kuendela kuishi. Kuna mambo mengi ya kuchagua ambayo yasingeweza kufikiriwa na watu wa zamani, lakini pia kuna changamoto za maisha ambazo watu wa zamani hawakukabiliana nazo - kuenea kwa virusi vya HIV na UKIMWI, kuvunjika kwa ndoa. Pengine huwezi kuhangaishwa na vyakula vinavyotia unajisi kama vile Danieli alivyofanya. Hata hivyo, kama vile Danieli na rafiki zake watatu, utakabiliwa na maamuzi juu ya kuutunza mwili wako usitiwe unajisi. Unaweza kumtumaini Mungu kwa ajili ya maisha yako ya usoni kwa kutii amri zake na kusubiri baraka zake katika maisha yako. Ama unaweza kuamua kufanya kama vile upendavyo. Jipe moyo kwa vile katikati ya maamuzi haya, ahadi za Mungu ni za kweli kama vile zilivyokuwa katika siku zile za Danieli na rafiki zake. Fikiria ahadi hizi zifuatazo • "Kwa maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho." (Jeremia 29:11) • "Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu, mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao." (1 Wakorintho 2:9) • "Kwa maana mimi, BWANA, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia." (Isaya 41:13) • Yesu alisema, "…Mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele." (Yohana 10:10) KUTUMIANENO LAMUNGU KATIKAMAISHAYAKO 1. Chukua ahadi moja kutoka katika orodha ya ahadi iliyo hapo juu na uikariri ili uwe tayari kuikumbuka wakati utakapotakiwa kufanya uamuzi fulani katika maisha yako. 2. Chukua muda kuandika baadhi ya ndoto ulizo nazo. Fikiri juu ya maamuzi fulani ambayo unaweza kuyafanya katika siku za usoni ili uweze kutimiza ndoto zako. Omba na kukabidhi ndoto hizo mbele za Bwana, mwombe akuongoze kufanya maamuzi ya busara.
Ukichagua kufanya mapenzi kabla ya ndoa unaweza kupata UKIMWI kitu ambacho kitakufanya usiishi muda mrefu hadi pale utakapowaona watoto au wajukuu wako. Kufanya uchaguzi si kitu rahisi sana kama vile ambavyo mtu anaweza kufikiria. Wakati mwingine inaonekana kana kwamba kuna mambo mengi ya kuchagua; wakati mwingine kuona kwamba hakuna uchaguo mzuri hata kidogo. Ni mambo gani yanayoweza kukusaidia kufanya uchaguo utakaokusadia utimize ndoto zako? Hizi ni hatua ambazo zinaweza kukusaidia kuamua 1. Orodhesha mambo unayopenda kuchagua Chukua muda kuandika mambo kadhaa unayoweza kuamua kulingana na uamuzi wako utakavyokuwa katika miaka kadhaa ya usoni. Kwa mfano, rafiki yako ameamua kwenda jijini kutafuta kazi na akataka aende pamoja nawe. Mambo gani yaweza kukukabili katika kufanya uamuzi huo? Moja ni kukubali kwenda pamoja na rafiki yako na lingine ni kubaki nyumbani. 1. Fikiria juu ya matokeo mazuri ama mabaya ya kila jambo. Andika matokeo mazuri ama mabaya katika kila uchaguzi ulioandika hapo juu. Kwa mara nyingine tena, yaandike mambo hayo ili uweze kulinganisha kwa urahisi. Je! Kutakuwa na matokeo gani ukienda mjini? Unaweza kupata kazi na kujipatia fedha. Unaweza kuendelea kuishi na rafiki yako atakayekusaidia. Je! Kuna madhara gani yatakayokupata? Utatengana na familia yako. Yawezekana usipate kazi. Utahangaika kupata chakula. 3. Jaribu kufahamu neno la Mungu linavyosema juu ya uamuzi wako Neno la Mungu linatupatia mwongozo wa kila hali inayotukabili. Katika hadithi ya Danieli na rafiki zake tunaona hawakufanya kitu rahisi, lakini pia walifanya kitu sahihi. Mungu aliubariki uchaguo wao mgumu walioufanya. Kutokana na mfano huo, uchaguo sahihi kwako ni upi? 4. Tafuta ushauri wa busara! Chukua muda kuzungumza na watu mbali mbali wanaokufahamu vizuri na unaowathamini kama vile wazazi, shangazi au mjomba, mchungaji, au rafiki yako mzuri juu ya mambo mbali mbali unayoweza kuchagua. Kubali wakuulize maswali kulingana na uamuzi wako. Wanaweza kuwa na mawazo mengine ambayo hukuwa umeyafikiria. 5. Omba Kumbuka kuwa hakuna uamuzi ulio mdogo hata usiweze kuuombea mbele za Mungu (Wafilipi 4:6-7). Usisumbuke iwapo hutapata majibu kulingana na vile ulivyofikiri au kulingana na vile wengine wanavyofanya. Endelea kuleta maswali yako mbele za Mungu naye atakuwa mwaminifu kukujibu kwa njia zake ambao huwezi kutarajia kwa kubadilisha mambo fulani katika maisha, kwa kuubadilisha mtazamo wako ama kwa kuwatumia watu wengine katika maisha yako. Wakati mwingine jibu laweza kuwa "hapana" ama "subiri." Ahadi ya Mungu juu ya maisha yako Ni jambo la kupendeza kuendela kuishi. Kuna mambo mengi ya kuchagua ambayo yasingeweza kufikiriwa na watu wa zamani, lakini pia kuna changamoto za maisha ambazo watu wa zamani hawakukabiliana nazo - kuenea kwa virusi vya HIV na UKIMWI, kuvunjika kwa ndoa. Pengine huwezi kuhangaishwa na vyakula vinavyotia unajisi kama vile Danieli alivyofanya. Hata hivyo, kama vile Danieli na rafiki zake watatu, utakabiliwa na maamuzi juu ya kuutunza mwili wako usitiwe unajisi. Unaweza kumtumaini Mungu kwa ajili ya maisha yako ya usoni kwa kutii amri zake na kusubiri baraka zake katika maisha yako. Ama unaweza kuamua kufanya kama vile upendavyo. Jipe moyo kwa vile katikati ya maamuzi haya, ahadi za Mungu ni za kweli kama vile zilivyokuwa katika siku zile za Danieli na rafiki zake. Fikiria ahadi hizi zifuatazo • "Kwa maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani, wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho." (Jeremia 29:11) • "Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu, mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao." (1 Wakorintho 2:9) • "Kwa maana mimi, BWANA, Mungu wako, nitakushika mkono wako wa kuume, nikikuambia, Usiogope; mimi nitakusaidia." (Isaya 41:13) • Yesu alisema, "…Mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele." (Yohana 10:10) KUTUMIANENO LAMUNGU KATIKAMAISHAYAKO 1. Chukua ahadi moja kutoka katika orodha ya ahadi iliyo hapo juu na uikariri ili uwe tayari kuikumbuka wakati utakapotakiwa kufanya uamuzi fulani katika maisha yako. 2. Chukua muda kuandika baadhi ya ndoto ulizo nazo. Fikiri juu ya maamuzi fulani ambayo unaweza kuyafanya katika siku za usoni ili uweze kutimiza ndoto zako. Omba na kukabidhi ndoto hizo mbele za Bwana, mwombe akuongoze kufanya maamuzi ya busara.
Itaendelea Juma nne
kama una ushauri maoni Habari tupigie au tuma ujumbe whatsapp 0769436440
download apps ya 4sn news usipitwe na vitu vizuri mda wote tuko na wewe kukuletea kilicho bora
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:
Post a Comment