Marekani yakatiza ufadhili kwa UNFPA linalohusika na mpango wa uzazi
Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGESImage captionUNFPA huhimiza afya ya uzazi na mpango wa uzazi katika takriban nchi 150 duniani
Marekani imesitisha ufadhili kwa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa idadi ya watu, UNFPA unaotoa msaada kwa ajili ya mpango wa uzazi kote duniani.
Hatua hiyo italifanya shirika hilo la Umoja wa Mataifa kupoteza takriban dola milioni thelathini za ufadhili kwa mwaka huu pekee.
UNFPA limepinga madai kuwa linafadhilili shughuli za uaviaji mimba.
Trump kuteua jaji anayepinga uavyaji mimbaUavyaji mimba: Wachangisha fedha kupinga sheria ya TrumpTrump hayuko juu ya sheria, jaji asema
Hili ni shirika la kwanza la Umoja wa mataifa kukabiliwa na kupunguwa kwa ufadhili baada ya ahadi ya kupunguza msaada wa kifedha kutoka kwa utawala wa Trump.
Haki miliki ya pichaGETTY IMAGESImage captionBalozi wa Marekani kwa Umoja wa mataifa Nikki Haley anasimamia uwezekano wa kupunguza ufadhili kwa Umoja huo
Hii ina maana kuwa UNFPA litapoteza ufadhili wa siku zijazo zikiwemo dola milioni 32.5 zilizokuwa zimepangwa kutumiwa mwaka huu.
Wizara ya mambo ya nje Marekani inasema kuwa uamuzi huo ulizingatia shughuli za UNFPA za mpango wake wa uzazi na serikali ya Uchina, ambazo inasema ulisaidia kuavya mimba na kufunga uzazi kwa lzima.
Sheria ya kupiga marufuku punyeto bungeni MarekaniTrump hajui apeleke wapi mshahara wakeWatakaoumia na watakaofaidi chini ya Trump Marekani
Badala yake ufadhili huo utaelekezwa katika mipango mingine ya uzazi katika nchi zinazoendelea.
Shirika hilo hatahivyo limesema kuwa madai hayo ''si sahihi'', na kwamba kazi zake zote zimekuwa ni za kuboresha haki za kibinfasi na wanandoa kuchukua maamuzi yao bila ubaguzi.
Mshirikishe mwenzako

No comments:
Post a Comment