» » CCM Yatoa Onyo kwa makada wake Wanaolalamika Baada ya Kutumbuliwa na Rais

CCM Yatoa Onyo kwa makada wake Wanaolalamika Baada ya Kutumbuliwa na Rais

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka na kukemea vikali kauli zinazotolewa na viongozi au makada wa chama hicho wambao wametenguliwa na Rais Dkt John Pombe Magufuli katika nafasi zao mbalimbali walizokuwa wakishikilia.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Siasa na Uhusiano wa Kimataifa, Kanali Mstaafu Ngemela Lubinga aliyasema hayo juzi akizungumza Mjini Iringa katika mkutano na wanafunzi wa vyuo vikuu vilivyomo mkoani humo ambao ni wananchama na pia viongozi wa chama hicho katika ngazi ya matawi na kata.

Lubinga aliwataka makada hao walioteuliwa na kisha kutemwa na Rais Dkt Mwagufuli ambaye pia ni Mwenyeketi wa CCM Taifa, kuacha kulalamika na kupiga kelele badala yake wakubiliane na mabadiliko hayo kwa nia ya kuheshimu maamuzi ya Ikulu kwa uamuzi uliochukuliwa dhidi yao.

Licha ya kuwa kiongozi huyo hakutaja majina ya viongozi aliowataka kuheshimu maamuzi ya Ikulu, lakini ni dhahiri kuwa miongoni mwa waliolengwa ni Mbunge wa Mtama (CCM), Nape Moses Nnauye ambaye alitenguliwa katika nafasi yake aliyokuwa ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo nafasi aliyoitumikia kwa kipindi cha miezi 15.

Nape alitenguliwa katika nafasi hiyo ikiwa ni saa chache tu tangu alipopokea ripoti ya kuvamiwa kwa kituo cha Clouds Media Group ambapo ripoti hiyo ilithibitisha kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam ndiye aliyehusika katika tukio hilo.

Nafasi ya Nape ilichukuliwa na aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Harrison George Mwakyembe ambaye naye nafasi yake ikajazwa na Mbunge wa kuteuliwa na Rais, Prof. Palamagamba Aidan John Kabudi ambaye ni mbobezi katika taaluma ya sheria.

Mwingine ambaye licha ya kuwa hakuenguliwa na Rais moja kwa moja lakini alionyesha kutoridhishwa na mchakato wa kuenguliwa kwake ndani ya CCM ni aliyekuwa Mbunge wa Bunge la Afrika Mashariki, Shyrose Bhanji. Yeye alienguliwa alipotaka kugombea kwa mara ya pili, na tangu hapo amekuwa akilalamika kwa madai  kuwa njia zilizotumika hazikuwa za haki.

“Rais anapoteua kiongozi na kumpa dhamana ni kwamba anaona kuwa unahitajika, lakini inapofika mahali amekuondoa ujue mazingira yale huwezi kuyamudu na anakuokoa ili usipate laana. Baadhi ya viongozi wameondolewa madarakani, lakini wamebaki wakilalamika mitaani ovyo.”  alisema Kanali Lubinga.

Lubinga alisema kuwa chama hicho sasa kimejikita kuhakikisha kuwa kinarejesha nidhamu na uwajibikaji ndani ya chama na serikali ili viongozi wote waliochaguliwa na kuteuliwa wafanye kazi kwa maslahi mapana ya taifa na wananchi.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...