» » Angalia Marekani inavyo imarisha vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini

Marekani kuimarisha vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini


Taifa la Korea kaskazini limekuwa likitoa picha kuhusu zoezi la kijeshiHaki miliki ya pichaAFP
Image captionTaifa la Korea kaskazini limekuwa likitoa picha kuhusu zoezi la kijeshi
Mamlaka ya rais Donald Trump imewaelezea maseneta wote 100 wa bunge la taifa hilo kuhusu tishio la Korea Kaskazini na kubaini mikakati ya kuishinikiza Pyongyang kupitia vikwazo vya kiuchumi na vile vya kidiplomasia.
Lengo ni kuilazimu Korea Kaskazini kusitisha mpango wa makombora ya masafa marefu pampja na ule wa Kinyuklia.
Mwandishi wa BBC mjini Washington anasema kuwa mkakati muhimu pia utakuwa kuirai China kuishinikiza Pyongyang.
Maseneta wa Marekani walielezwa na mamlaka ya rais Trump kuhusu tishio linaloletwa na Korea KaskaziniHaki miliki ya pichaEPA
Image captionMaseneta wa Marekani walielezwa na mamlaka ya rais Trump kuhusu tishio linaloletwa na Korea Kaskazini
Seneta mmoja alisema kuwa habari hiyo kuhusu Korea Kaskazini ilikuwa muhimu sana.
Taarifa iliotolewa kwa niaba ya wizara ya Ulinzi na ile ya kigeni ilisema kuwa Marekani bado itaendelea na mazungumzo lakini imejiandaa kujitetea pamoja na washirika wake.
Awali kamanda mkuu wa Marekani katika eneo la Pacific alitetea kupelekwa kwa mfumo wa silaha za kisasa nchini Korea Kusini.
Hali ya wasiwasi imepanda huku kukiwa na hofu kwamba Korea Kaskazini inapanga kujaribu makombora mapya.
''Marekani inataka uthabiti na kutoenea kwa silaha za kinyuklia katika rasi ya Korea'', ilisema taarifa ya pamoja iliotolewa na waziri wa maswala ya kigeni REx Tillerson, waziri wa Ulinzi Jim Mattis na Mkurugenzi wa maswala ya ya ujasusi Dan Coats.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...