» » Alicho sema Mbunge Lijuakali Baada ya Kuachiwa Huru na Mahakama

Alicho sema Mbunge Lijuakali Baada ya Kuachiwa Huru na Mahakama

Mbunge wa Kilombero kupitia chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Peter Lijualikali jana amefanikiwa kuachiwa huru na maafisa wa gereza la Ukonga baada ya kukamilisha taratibu za kutoka gerezani.

Akizungumza mara baada ya kutoka gerezani Mbunge Lijualikali aliwataka watanzania kutumia demokrasia ya kweli katika kutafuta majawabu ya matatizo waliyonayo ili kubadili taswira ya  Tanzania na kuwa nchi ya maendeleo na kuongeza mshikamano bila kubaguana.

Kwa upande wake baba mzazi wa Mbunge huyo Amberose Lijualikali aliviomba vyombo vya dola nchini kufuata sheria za nchi zinavyoelekeza katika kutoa maamuzi.

Kwa upande wake Waziri Mkuu Mstaafu na Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Pwani Mhe. Fredrick Sumaye aliyekuwepo katika gereza la Ukonga Dar es Salaam wakati mbunge huyo akiachiwa, aliwataka viongozi na watanzania kutumia demokrasia katika kudai haki zao ili kulinda amani ya nchi iliyopo.

Hukumu ya Lijualikali ilitenguliwa jana na Mahakama Kuu baada ya kukaa gerezani kwa zaidi ya siku 70 akituhumiwa kufanya vurugu katika uchaguzi wa mwaka 2015. Katika hukumu hiyo, Lijualikali alihukumiwa bila kupewa masharti ya faini.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles