» » Waziri aliyefutwa Tanzania Nape Nnauye asema alijua kuna gharama

Waziri aliyefutwa Tanzania Nape Nnauye asema alijua kuna gharama


Waziri aliyefutwa Tanzania Nape Nnauye asema alijua 'angelipia gharama'
Aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye alihuhutubia waandishi wa habari leo akiwa chini ya vyombo vya usalama na kutetea msimamo wake.
Taharuki ilitokea mara baada ya waandishi wa habari kupata taarifa kuwa kikao kilichoandaliwa na aliyekuwa waziri wa habari hakipo tena, lakini dakika chache baadae Nape aliandika katika kurasa yake ya Twitter kuwa yuko njiani na kikao kipo palepale.
Nape alipofika karibu na eneo la kikao alizuiwa na askari kutoka katika gari lake huku wakimshika kwa nguvu na kumtishia kwa kumnyooshea bunduki.
Hali hiyo ilimfanya Nape kuongea kwa hasira akitaka kujua nia ya askari hao kumnyooshea bunduki, huku kundi kubwa la waandishi wa habari wakipiga kelele wakitaka askari hao wamuachie Nape aongee.
Nape alianza kwa kusema nia yake ilikuwa ni kutaka kuwatuliza wananchi watulie kwa sababu wakati anateuliwa hakuulizwa na hata sasa ameachishwa hajaulizwa na yeye hana kinyongo na rais wake.
Ingawa aliendelea kuzungumza kwa hasira alisema haogopi chochote.
"Jana wakati narudisha ripoti kuhusu mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuvamia kituo cha habari cha habari cha Clouds, nilijua kuwa kuna gharama ya kuilipa," alisema Bw Nnauye.
"Hivyo nashangaa kwa nini vyombo vya usalama 'wanapaniki', kwa nini watu 'wanapaniki'. Nape ni mtu mdogo tu ila tuhangaike na Tanzania yetu, mimi nmesimamia ukweli tu, Kinachokutanisha watu ni ukweli na sio fitina. Vijana wenzangu wa Kitanzania simamieni ukweli".
Hata hivyo aliongeza kwa kusema kuwa lengo la kuja kuzungumza hapo ni kumshukuru rais kwa kumwamini kumpa nafasi hiyo kwa kipindi cha mwaka mmoja.
Bw Nnauye akihutubia wanahabari Dar es Salaam
Aidha, alimpongeza waziri mpya aliyechaguliwa, Dkt Harrison Mwakyembe, kwa kuwa ni mwanasheria na ana taaluma ya habari.
Nape
Image captionWaandishi wa habari wakijaribu kupata habari kutoka kwa Bw Nnauye
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440






BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en





tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...