» » Urusi na China zatumia kura ya turufu kuisaidia Syria

Urusi na China zatumia kura ya turufu kuisaidia Syria

Haki miliki ya pichaREUTERSImage captionWachunguzi wa UN, juu ya Syria

Urusi na China zimetumia kura ya turufu kuzuia jaribio la Umoja wa Mataifa la kutaka kuiwekea vikwazo serikali ya Syria.

Marekani, Uingereza na nchi nyengine katika Baraza la Usalama, zilitaka kuiadhibu Damascus kwa tuhuma za kutumia silaha za sumu katika maeneo ya waasi.

Ni mara ya saba sasa Urusi inatumia kura yake ya VETO kuikinga serikali ya Rais Assad na tuhuma za kimataifa.

Katika hotuba yake iliyojawa hisia kabla ya kura, balozi wa Uingereza katika Umoja wa Mataifa, Matthew Rycroft, alisimulia kifo cha mwathirika mmoja ambae alipelekwa katika hospitali baada ya shambulio la gesi yenye sumu.

Hata hivyo, kwa upande wake, balozi wa China katika Umoja wa Mataifa, Liu Jieyi, ameliambia Baraza la Usalama kwamba bado hakuna vilelezo kwamba serikali ya Syria imetumia silaha za kemikali.

Naye Rais Vladmir Putin amesema vikwazo vitazuia jitihada za mazungumzo ya amani yanayoendelea Geneva baina ya serikali na wapinzani wake.

Marekani imesema Urusi na China zimekataa kuwajibisha vikosi ambavyo viliangusha gesi za sumu na kusababisha vifo vya wanaume, wanawake na watoto.

Mshirikishe mwenzako 

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...