» » USHINDI HATIMAYE- SOMO: NAMNA YA KUREJESHA-3

USHINDI HATIMAYE- NAMNA YA KUREJESHA-3
Picha ya Kirumba Seventh-day Adventist Church
MHUBIRI: Mchungaji David Mbaga
MAHALI: Kanisa la Waadventista Wasabato Mabatini Mwanza
MAFUNGU: Walawi 11; Kumbukumbu ya torati14; Walawi 7:22-24;
“Mlapo mnywapo au mtendapo neno lolote, fanyeni yote kwa utukufu wa Mungu" (1 Wakorintho 10:31).
Sokwe hajawahi kubadili mfumo wake wa kula,lakini mwanadamu mwenye akili timamu amepotea kabisa.
Mungu hajakunyima chakula,chakula kipo,ametupa maelekezo bora ya kutunza afya zetu kwa kanuni ya vyakula bora kiafya na namna mtindo wa maisha wapaswa uwe. Vyakula anavyotuambia kuwa tunaruhusiwa kuvila ni vyema sana kwetu na vinatusaidia katika ukuaji wa kiroho na kimwili. Vyakula anavyotuambia tusivile vinatufanya kushambuliwe na magonjwa.
Biblia katika Kumbukumbu la Torati 14 Mambo ya Walawi 11 ina orodha ya ndege, wanyama, na samaki ambao Mungu alisema hawafai kuliwa. Kwa mujibu wa sura hizo, wanyama safi ni lazima kwato zao zigawanyike na pia wacheue. Samaki safi ni lazima wawe na magamba na mapezi, vyote viwili. Ndege wanaokula uchafu,nguruwe,sungura,wibari, samaki wakiwemo papa,katfish, nyangumi, pomboo, dagaa kamba, kaa, kambakoche, chaza mdogo, chaza mkubwa, na wengine wengi ni najisi,haramu ni machukizo kwa Mungu.
Watu wanaokula chakula cha mimea wana afya bora zaidi, tena wanaishi kwa muda mrefu zaidi.Wataalamu wengi wa mambo ya afya na lishe wanatushauri kutumia chakula kile cha awali walichopewa wanadamu cha kokwa, nafaka na matunda pamoja na mbogamboga kwaajili ya ustawi wa afya zetu. Wanadamu katika matumizi mabaya ya biblia Marko7:14-15, 18-21, ndani ya moyo hutoka mawazo machafu. Biblia katika Mwanzo 9:4 “Bali nyama pamoja na uhai, yaani, damu yake, msile.”
Thamani ya mwili wako haifananishwi na kitu chochote,tutunze miili yetu.Tusiingize taka katika miili yetu,fedha na mali ulizonazo hazina thamani kulinganisha na mwili ulioumbwa na Mungu kwa mfano wake.Mwili ni hekalu la Roho Mtakatifu tumeagizwa tuutunze.Masikio urembo husikia chochote.
Mtu muadilifu huisikia sauti ya Mungu na kumfuate popote aendako. Bwana yu karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.Atawafanyia wamchao matakwa yao, Naye atakisikia kilio chao na kuwaokoa.Amen
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...