» » Uganda yaongoza kwa ufasaha wa lugha ya kiingereza Afrika

Uganda yaongoza kwa ufasaha wa lugha ya kiingereza Afrika

Uganda imetajwa kuwa nchi yenye raia wanaozungumza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha barani Afrika.
Utafiti uliofanywa na shirika la lugha duniani World Linguistic Society umesema Uganda inaongoza ikifuatiwa na Zambia halafu Afrika Kusini ikiwa katika nafasi ya tatu na Kenya katika nafasi nne.
Uganda imetajwa kuwa nchi yenye raia wanaozungumza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha zaidi barani Afrika
Image captionUganda imetajwa kuwa nchi yenye raia wanaozungumza lugha ya Kiingereza kwa ufasaha zaidi barani Afrika
Kulingana na gazeti la The New Vison nchini Uganda, utafiti huo unajiri kufuatia kanda ya video iliomuonyesha malkia wa urembo kutoka Rwanda akishindwa kujielezea kiingereza.
The New Vison linasema kuwa mwaka 2015, mmoja wa malkia hao wa Urembo katika shindano la Malkia wa urembo nchini Rwanda Uwase Honorine alishindwa kujibu maswali aliyoulizwa na majaji wa shindano hilo.
Rwanda iliokuwa chini ya koloni ya Ufaransa ilianza kuzungumza Kiingereza baada ya kukosana na Ufaransa.
Gazeti la The New Vision linasema kuwa kiingereza nchini Uganda ndio lugha rasmi, na ndio lugha inayotumiwa katika shule na taasisi tofauti nchini humo.
Watoto huanza kujifunza lugha hiyo katika shule za msingi.
The New Vison linasema kuwa hivi majuzi serikali iliziagiza shule kufunza lugha za nyumbani kwa wale wanaosoma katika shule za msingi lakini ikasisitizia kuwa Kiingereza ndio lugha itakayotumiwa katika mtaala.
Mataifa yanayozungumza kiingereza kwa ufasaha:
1.Uganda
2. Zambia
3. South Africa
4 . Kenya
5. Zimbabwe
6. Malawi
7. Ghana
8. Botswana
9. Sudan
BONYEZA HAPA -Download App ya 4SN NEWS


Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...