» » Umeisikia hii kuhusu Mkwasa na Yanga


Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Tanzania Charles Boniface Mkwasa
Klabu ya Yanga inatajwa kuwa kwenye mazungumzo na kocha wao wa zamani Charles Boniface Mkwasa kwa ajili ya kumrudisha kwenye benchi la ufundi la klabu hiyo.
Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya Yanga kimeiambia shaffihdauda.co.tz kuwa, kuna uwezekano mkubwa Mkwasa akarejea kwenye benchi la ufundi la Yanga.
“Uongozi wa Yanga tayari umeanza mazungumzo na Mkwasa kwa ajili ya kumrudisha kwenye benchi la ufundi baada ya kuachana na timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’.”
Mkwasa ambaye aliondoka Yanga akiwa kocha msaidizi wa Hans van Pluijm kwenda kuifundisha Taifa Stars, baada ya TFF kumfukuza aliyekuwa kocha wa timu hiyo Mart Nooij.
Juma lililopita TFF ilitangaza kuachana na Mkwasa baada ya pande mbili kufikia makubaliano ya kuvunja mkataba, swali linalobaki ni kwamba, Mkwasa akirudi Yanga ndio mwisho wa Mwambusi?

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles