» » Ubuyu wa Moto Moto!! Huyu Ndiye Waziri wa Magufuli Anayechepuka na Flora Mvungi,Walikutana Dodoma,Flora Akiri Kila Kitu Bila Kukataa

HUKU kukiwa na taarifa kwamba ndoa yake na msanii wa Bongo Fleva, Hamis Ramadhan Baba ‘H-Baba’ imeparaganyika, mrembo wa Bongo Movies, Flora Mvungi amedaiwa kunasa kwenye penzi la mmoja wa mawaziri wa serikali ya awamu ya tano.

 
Chanzo kilicho karibu na msanii huyo kimepenyeza habari kuwa, mrembo huyo kwa sasa yupo chini ya himaya ya waziri huyo (jina kapuni kwa kuwa hatujampata) ambapo safari ya uhusiano wao ilianzia mjini Dodoma.
“Nakumbuka ilikuwa ni mwaka jana, Flora alienda Dodoma na wasanii wenzake sasa alipofika mjengoni, waziri aliuona
mzigo hivyo akaomba nafasi na Flora bila hiyana akakubali.
“Mwanzoni kidogo alichomoachomoa lakini waziri alimuahidi maisha mazuri, na kwa kuwa tayari walikuwa kwenye gogoro na mtu wake(H-Baba), ilikuwa ni kama kumsukuma mlevi tu. Mtoto wa kike akaingia mzimamzima, yani sasa hivi Flora, kafa kaoza kwa mheshimiwa,” kilisema chanzo hicho makini.
Jitihada za kumpata waziri huyo ziligonga mwamba kufuatia simu yake ya mkononi kutokuwa hewani. Atakapopatikana, tutaripoti kwa upande wake ili kujua anazungumziaje madai hayo.
Kwa upande wake Flora, alipotafutwa na mwanahabari wetu alikiri kukutana na waziri huyo Dodoma lakini akaomba asizungumzie suala hilo kwani litamweka kwenye nafasi mbaya katika jamii.
“Naomba sana mliache hilo suala, najua aliyevujisha lakini nawaombeni sana mliache kabisa. Litanichafua tafadhalini sana,” alisema Flora.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...