» » TP Mazembe yamrudisha Mputu, yawaongezea mikataba nyota wake tegemeo




TP Mazembe imefanikiwa kumrudisha kundini nyota wake wa zamani, Tresor Mputu baada ya kushinda kesi dhidi ya klabu ya Kabuscorp ya Angola.

Mputu alishindwa kucheza kwa muda mrefu baada ya kuondoka Kabuscorp ambayo ilidai amevunja mkataba.

Baada ya juhudi kubwa za rais wa TP Mazembe, Moise Katumbi ambaye alituma wawakilishi wake FIFA,Mputu ameishinda kesi hio na Kabuscorp wameamuliwa kuwalipa TP Mazembe dola milioni 1.5 iliyokuwa ada ya uhamisho wake.

FIFA imeliarifu shirikisho la mpira la JK Kongo, FECOFA kumuidhinisha Mputu kuichezea TP Mazembe kwa mara nyingine.

Mputu anakumbukwa na wengi kwa kuiongoza TP Mazembe kuwa klabu ya kwanza Afrika kufika fainali za Klabu Bingwa Duniani mwaka 2010 walipofungwa na Inter Milan.

Kwa upande mwingine, TP Mazembe imewaongezea mikataba nyota wake, Jonathan Bolingi na Rainford Kalaba.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles