» » Picha: Mamilioni ya wanawake duniani waandamana kupinga Urais wa Donald Trump


Rais Donld Trump aliapishwa Ijumaa hii kwa sherehe mjini Washington DC, lakini hiyo haimaanishi kuwa mambo yametulia – ndio yameanza.

Jumamosi hii, mamilioni ya wanawake duniani, waliandamana kupinga kuapishwa kwake kama rais wa 45 wa Marekani. Maandamano makubwa zaidi yalikuwa Marekani hususan kwenye mji mkuu, Washington.

Wanawake hao walioungwa mkono na mastaa kibao pamoja na wanaume walioependa kuwaunga mkono, walikuwa na ujumbe mmoja tu, kuwa hawatakuwa kimya kwa miaka minne yote ya uongozi wa Trump.
 
Kulikuwa na maandamano kwenye zaidi ya miji 600 duniani kote huku waandamaji wakiwa na mabango mengi yanayomdhihaki na kumlaani Trump.

Mastaa walioshiriki kwenye maandamano hayo ni pamoja na Katy Perry, Madonna, Scarlett Johansson, Jake Gyllenhaal, Emma Watson, Ashley Judd, Cher, America Ferrera, Kristen Stewart, Charlize Theron, Whoopi Goldberg, Cynthia Nixon, Charlotte Church, Yoko Ono, Helen Mirren, Julia Roberts, John Legend, Amy Schumer na wengine.

Takriban watu milioni 2.2 wanaaminika kuwa waliandamana kutetea haki zao na za binadamu.

Pamoja na miji mingi ya Marekani, miji mingine duniani iliyokuwa na maandamano makubwa ni pamoja na London, Paris, Berlin, Edinburgh, Rome, Prague, Amsterdam, Stockholm, Athens, Copenhagen, New Delhi, Brussels, Mexico City, Barcelona, Manila, Toronto, Madrid, Geneva, Cardiff na Sydney.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...