» » Orodha ya Vitu na Wanyama Vilivyopewa Jina la Obama Kwa Ajili ya Kumuenzi..!!!

BARACK Obama amestaafu nchini Marekani akiwa ameacha vitu kama maktaba, barabara na shule vikiwa vimepewa jina lake ikiwa ni ishara ya heshima aliyopewa na Wamarekani.
Kutakuwa na Maktaba ya Rais Barack Obama mjini Chicago. Pia kuna shule nyingi zilizopewa jina la kiongozi huyo wa kwanza Mwamerika Mweusi nchini humo.
Mbali na hayo, kuna vitu vingi ambavyo huwezi kutarajia vilivyopewa jina lake ikiwamo vimelea na buibui.
 Kimelea
Kuna mnyoo aina ya Baracktrema obamai, ambao umepewa jina la Rais Barack Obama
Mnyoo huo ambao kisayansi huitwa Baracktrema obamai ni kimelea cha pili kupewa jina la Obama.
Mnyoo huu ni mrefu na unafanana na uzi, huambukiza kasa wa maji yasiyo na chumvi Malaysia na unaweza kuua.
“Hili ni jambo jema bila shaka, tumefanya hivi kwa heshima ya rais wetu mstaafu,” anasema Dk. Thomas R Platt, ambaye ni mtaalamu wa vimelea wa kasa na mgunduzi wa aina hiyo ya mnyoo.
Mbali na mnyoo huo, watafiti waliwahi kuupa mnyoo unaopatikana nchini Kenya jina la Paragordius obamai, ambao uligunduliwa karibu na nyumbani kwa Obama.
Samaki
Samaki anayepatikana katika hifadhi ya viumbe wa baharini ya Papahanaumokuakea.
Ikiwa ni sehemu ya kutoa heshima kwa Obama kwa juhudi zake za uhifadhi wa viumbe wa baharini katika Bahari ya Pasifiki. Wanasayansi walimpa samaki mmoja anayepatikana eneo la Kure Atoll katika hifadhi ya Papahānaumokuākea, pwani ya Hawaii jina la rais huyo. Samaki huyo ana rangi ya damu ya mzee na dhahabu.
Mwaka 2012, watafiti walimpa jina Etheostoma Obama samaki mwingine wa rangi ya samawati na manjano. Samaki huyo hupatikana katika mito ya Duck na Buffalo inayotoa maji yake kutoka kwa Mto Tennessee.
 Mjusi
Mjusi mwenye urefu wa futi moja na aliyekuwa na meno yaliyosimama wima alipewa jina la Obamadon kutokana na tabasamu la Obama.
Mlima
Obama ni miongoni mwa marais wa Marekani ambao wana milima iliyopewa majina yao. Taifa la Antigua lilibadili jina la mlima mrefu zaidi nchini humo, mlima wa Boggy kuwa Mlima Obama.
 Kuvu
Mwaka 2007, watafiti walizipa kuvu (ukungu wa miti na miamba) jina Caloplaca obamae, pindi Obama alipoanza kufanya kampeni yake ya urais. Walichukua hatua hiyo kwa sababu ya Obama kuunga mkono masomo ya sayansi.
 Kituo cha mafuta
Kijiji cha Moneygall katika eneo la Offaly, katikati mwa Dublin na Limerick nchini Ireland, kuna kituo cha mafuta ambacho kilipewa jina la Obama.
Katika Barack Obama Plaza kuna kituo cha mafuta, mgahawa na kituo cha wageni ambacho hutoa habari kuhusu uhusiano wa Obama na Moneygall.
Kijiji cha Moneygall ndicho asili ya babake babu wa babu wa Rais Barack Obama.
 Mkate
Kabla ya Rais Obama kuzuru Ireland, waokaji wa mikate walikimbia kuoka mikate maalumu.
Mkazi wa Moneygall, Joseph Kearney aliwasilisha mikate maalumu kwa majamaa wa Obama nchini Ireland waliokuwa wakijiandaa kwa ziara yake.
Haijulikani iwapo Obama alikula mikate hiyo au la.
 Ndege
Kuna ndege anayepatikana Amazon magharibi ambaye amepewa jina Nystalus obamai.
 Shule Kenya
Katika kijiji cha Kogelo, alikozaliwa baba yake Obama, kuna shule mbili, Shule ya Msingi Senator Obama Kogelo na Shule ya Sekondari Senator Obama Kogelo.
Zilipewa majina hayo Obama alipokuwa seneta wa Illinois.
 Buibui
Kuna buibui anaitwa Aptostichus barackobamai wa aina ya trapdoor, ambao wamepewa jina hilo kutokana na Obama kuwa shabiki wa Spider-Man.
Wengine huitwa Aptostichus stephencolberti (kutokana na mchekeshaji Stephen Colbert) na Aptostichus angelinajolieae (kutokana na mwigizaji Angelina Jolie).

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...