» » KUTENGULIWA Mramba Sio Dawa' Habibu Mchange


Nafikiri kama taifa tumekwama.
Wanasiasa wetu hasa viongozi wa serikali hawaheshimu wataalam wala utaalam na wataalam wetu pamoja na wasomi wanaanza kuingia hofu na kutaka kuwafurahisha Wanasiasa.

Kwa mtazamo wangu, kumuondoa Mramba Tanesco sio suluhisho la tatizo la uendeshaji wa Tanesco.

Tanesco wanasema Gharama za uendeshaji wa shirika Hilo ni kubwa na linaizidi uwezo management.

Tanesco wanasema na ripoti kadhaa zinaonyesha kuwa Wana madeni makubwa.

Na bahati mbaya madeni hayo yamekuwa yakiongezeka siku hadi siku.

Ipo haja mahsusi ya serikali kuainisha chanzo kikuu cha kukua Kwa Gharama za uendeshaji Tanesco.

Ipo haja pia ya serikali kuangalia ukubwa huu wa madeni wanayodaiwa Tanesco na vyanzo vyake.

Hii kufurahia Fulani katumbuliwa bado haitoi jibu sahihi la Sababu za Tanesco kutaka kupandisha bei ya umeme.

Kama serikali isipochukua hatua mahsusi na madhubuti lazima bei ipande tu, kama sio Leo kesho na kama sio kesho kesho kutwa, itapanda tu.

Itapanda Kwa Sababu Tanesco wanahisi hiyo inaweza kuwa sehemu ya wao kuwasaidia kupunguza deni na kugharamia uendeshaji wao.

Ushauri wangu ni Serikali kupitia upya mikataba yote inayoipa mzigo wa madeni Tanesco.

Waipitie na watujulishe Watanzania kupitia wawakilishi wetu au moja Kwa moja kila aina ya mkataba na changamoto zake.

Kisha kama taifa tupige mstari na kuweka way foward ya pamoja.

Kinyume na hapo Leo Mramba katenguliwa, na kesho mwengine atatenguliwa na kutenguliwa na kutenguliwa.

Lakini je kutenguliwa huku kunajibu Sababu za wao kupandisha bei? ...

Kuna haja Sasa ya sisi kama Taifa kutibu chanzo cha tatizo sio kuhangaika na matokeo ya tatizo.

Habibu Mchange
Mwananchi.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...