» »Unlabelled » Watu 50 wauawa kwenye mapigano Malakal, Sudan Kusini

Watu 50 wauawa kwenye mapigano Malakal, Sudan Kusini


Dkt Riek Machar na Rais Salva KiirImage copyrightAFP
Image captionUhasama kati ya Dkt Riek Machar na Rais Salva Kiir uliibuka tena Julai mwaka huu
Zaidi ya watu 50 wanaripotiwa kuuawa kufuatia mapigano mapya yaliyozuka nje ya mji wa Malakal nchini Sudan Kusini.
Vikosi vya waasi viliendesha mashambulizi kwenye mji huo wa pili kwa ukubwa siku ya Ijumaa, baada ya kuteka vijiji vilivyo karibu.
Hata hivyo serikali inasema kuwa wanajeshi wake wamewatimua waasi hao hatua iliyosababisha maafa mengi.
Sudan Kusini imekumbwa na misukosuko tangu kujipatia uhuru 2011Image copyrightAFP
Image captionSudan Kusini imekumbwa na misukosuko tangu kujipatia uhuru 2011
Msemaji wa waasi aliliambia shirika la habari la Reuters kuwa wana matumaini ya kuteka mji wa Malakal na kuongeza kuwa hakuna matumaini ya kuwepo makubaliano kati ya kiongozi wao Riek Machar na rais Salva Kiir pamoja na kati ya kabila la Nuer na lile la Dinka.
Asante kwa kutembelea Blog yetu washirikishe na wenzako, Pia tunaomba maoni yako hapa au tupigie kwa (+255) 0769436440 Karibu Tena

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles