Vijana wakwamisha Uchaguzi DRC
Rais wa Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo Joseph Kabila ametupilia mbali shutuma kwamba amesogeza mbele tarehe ya uchaguzi ili aendelee kung'ang'ania madarakani.
Amesema serikali yake isingependa kuacha idadi kubwa ya wananchi wake na wengi wao wakiwa ni vijana ambao hawakujiandikisha kupiga kura na wakose haki yao ya kupiga kura .
Mwishoni mwa wiki iliyopita,kiongozi wa tume ya uchaguzi nchini Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo alitangaza uwezekano wa kusogezwa tarehe ya kupiga kura hadi hapo desemba 2018.
Siku za hivi karibuni Jamuhuri ya demokrasia ya Kongo imekuwa ikikumbwa na maandamano ya mara kwa mara ambayo yamekuwa yakilenga ucheleweshwaji wa uchaguzi nchini humo.
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

No comments:
Post a Comment