*K E S H A LA A S U B U H I*
JUMAPIL OCT-9/2016
*NENO KUU 👇🏽*
👉🏽 *TUNAKAA NDANI YA KRISTO 👇🏽*
👉🏽 *Mungu Anatupogoa Ili Kutufanya Tuzae Zaidi*
🍒🍒🍒🍒🍒🍒🍒🍒
*Fungu la maandiko 👇🏽*
👉🏽 *_📝Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa._* *YOHANA- 15:2.*
🍒🍒🍒🍒🍒🍒🍒🍒
*_▶Wale watakaoenenda wakifuata kwa karibu nyayo za Mkombozi wao mwenye kujitoa nafsi na kujikana nafsi, moyo wa Kristo utaakisiwa mioyoni mwao. Usafi na upendo wa Kristo vitang’aa katika maisha yao na tabia zao kila siku, wakati upole na ile kweli ikiongoza njiani mwao. Kila tawi lizaalo linapogolewa, ili lipate kuzaa matunda zaidi. Hata matawi yanayoweza kuzaa yanaweza kuonesha majani mengi sana na kuonekana kwa namna ile ambayo sivyo yalivyo kwa hakika. Wafuasi wa Kristo wanaweza kufanya kazi kwa ajili ya Bwana na bado wakawa wanafanya nusu ya kile ambacho wangeweza kufanya. Hivyo basi anawapogoa, kwa sababu kuipenda dunia, kuendekeza nafsi na kiburi vinaonekana maishani mwao. Wakulima hukata vikonyo vilivyozidi kwenye mzabibu…, kwa namna hiyo wakiifanya mizabibu kuzaa zaidi. Vitu hivi vinavyoweza kuwa vizuizi lazima viondolewe na hali ya ukuaji usio mzuri ukatiliwe mbali, ili kutoa nafasi kwa ajili ya mionzi inayoponya ya Jua la Haki…._*
*_▶Wengi hawaelewi kusudi ambalo kwa hilo waliumbwa. Lilikuwa ni kubariki binadamu na kumtukuza Mungu, badala ya kufurahia tu na kujitukuza nafsi. Mungu anadumu kupogoa watu wake, akikatilia mbali matawi yaliyozidi, yanayosambaa, ili wapate kuzaa matunda kwa utukufu wake na siyo kuzaa majani tu. Mungu anatumia huzuni kutupogoa, anatumia hali za kuvunja moyo na mateso ili ukuaji uliozidi wa mielekeo ya tabia zenye nguvu ambazo ni potovu ipate kudhoofishwa na tabia zilizo nzuri zaidi zipate nafasi ya kukua. Ni lazima sanamu ziachwe, dhamiri lazima ziwe pole zaidi, tafakuri za moyo lazima ziwe za kiroho na tabia nzima ipate kuwa na ulinganifu unaotakiwa._*
*_▶Kwa kukaa ndani ya Kristo, tunaweza kuwa na utamu wake, harufu yake nzuri, nuru yake….anayoing’aza mioyoni mwetu. Nuru yake iliyomo mioyoni mwetu itang’aa kutoka kwenye nyuso zetu. Kwa kudumu kutazama uzuri na utukufu wa Kristo, tunabadilishwa na kuwa sawa na mwonekano wake._*
………………………🔚……………………
*U B A R I K I W E*

No comments:
Post a Comment