» »Unlabelled » Wapinzani wanyimwa chakula Zimbabwe

Wapinzani wanyimwa chakula Zimbabwe


Mshirikishe mwenzako
Zimbabwe
Image captionRais Robert Gabriel Mugabe
Tume ya haki za binadamu nchini zimbabwe imesema kuwa watu wanaounga mkono upinzani, walio kwenye maeneo yenye ukame wamenyimwa misaada ya chakula na chama tawala cha ZANU-PF.
Mwenyekiti wa bodi maalum Elasto Mugwadi, amesema kuwa kwa sasa uchunguzi umebainisha kuwa watu wanaounga mkono upande wa upinzani wanaambiwa waziwazi kuwa hawatopewa msaada wowote wa chakula na inaarifiwa kuwa watu wengi wameathirika kutokana na hali hiyo.Taarifa ya serikali inaonyesha kuwa nusu ya wakazi wa vijijini wamekumbwa na njaa, jambo linalochochea kupingwa kwa utawala wa rais Mugabe.
Wakati huo huo mahakama kuu nchini humo imebatilisha marufuku ya maandamano yaliyokatazwa na polisi kwenye mji mkuu wa Harare. Ambapo marufuku hiyo ilidumu kwa muda wa wiki mbili.
Wanaharakati wanne wanaopinga utawala wa rais Mugabe ndiyo waliwashilisha pingamizi mahakamani kupinga uamuzi wa polisi kupiga marufuku maandamano kwenye mji mkuu wa Harare.
Hakimu wa mahakama kuu ya nchini humo amesema kuwa marufuku hiyo ya polisi ilikuwa batili. Siku za hivi karibuni kumekuewa na ongezeko la wimbi la maandamano nchini Zimbabwe, wakiandamana kuhusu mdororo wa uchumi nchini humo.
Maandamano makubwa yanaratibiwa na wanaharakati kupitia mitandao ya kijamii.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles