» »Unlabelled » Obama ayataka mataifa tajiri kusaidia wakimbizi

Obama ayataka mataifa tajiri kusaidia wakimbizi


Mshirikishe mwenzako
Mkimbizi wa SyriaImage copyrightREUTERS
Image captionMkimbizi wa Syria
Rais wa Marekani Barack Obama ameyataka mataifa tajiri kufanya kila linalowezekana kuwasaidia watu wanaokimbia vita.
Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano kuhusu wakimbizi katika Umoja wa Mataifa amekiri kuwa dunia inakabiliwa na changamoto nyingi.
Amezitaka nchi tajiri kuchukulia tatizo hilo kama ni la kwao na kuongeza kuwa tatizo la sasa la wakimbizi ni ishara ya vita na mateso na kwamba itaweza kushughulikiwa tu endapo migogoro kama ule wa Syria utamalizwa.
Aidha amezitaja nchi 50 zinazoshiriki mkutano huo kuwa zimeahidi kuchukua wakimbizi laki tatu na sitini elfu katika kipindi cha mwaka huu, ikiwa ni mara mbili ya idadi ya mwaka uliopita, huku Canada na Ujerumani zikiongoza.
Rais Obama pia ametangaza kwamba fedha zilizokuwa zikichangwa na mashirika ya kibinadamu na Umoja wa Mataifa zimeongezeka kwa dola ya Marekani bilioni nne nukta tano.
ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU WATARIFU NA WENZAKO PIA TUPIA MAONI YAKO

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles