» »Unlabelled » Mwanasoka wa Sierra Leone, Bah afariki kwenye ajali

Mwanasoka wa Sierra Leone, Bah afariki kwenye ajali


Mamadu Alphajor Bah (right)
Image captionMamadu Alphajor Bah alicheza soka ya kimataifa kwao Sierra Leone na vile vile UChina, UBelgiji na Korea kusini
Aliyekuwa mwanasoka wa kimataifa, raia wa Sierra Leone, Mamadu Alphajor Bah amefariki dunia katika ajali mbaya ya barabarani iliyofanyika karibu na mji mkuu wa nchi hiyo Freetown.
Gari la mchezaji huyo wa kiungo kati aliye na umwi wa miaka 39 liligongana na lori uso kwa uso wakati wa ajali hiyo.
Alikimbizwa hospitalini Goderich, lakini akafariki punde kutokana na kupoteza damu nyingi. Polisi wangali wanachunguza ajali hiyo.
Bah aliwahi kuichezea nchi yake Sierra Leone mara 25 katika mechi za kimataifa.
Mchezaji mashuhuri Mohamed Kallon, aliyekuwa nahodha wa timu hiyo wakati Bah alipokuwa angali anacheza, amelitaja tukio hilo kama pigo kuu.
" Bado nimeshikwa na mshtuko, na nina huzuni sana kumpoteza kaka na rafiki yangu Mamadu Alphajor Bah," Kallon ameiambia BBC. "Alikuwa mchezaji mwenye kipaji kizuri, mtu anaejituma, mcheshi , unaefurahiwa kuwa nae katika timu moja .
Mchezaji mwenzake mwengine Ibrahim Kargbo,nae amesema : 'Ni kama ndoto mbaya , kweli nimeshtuka, ni kaka ambae daima atakuwa nasi kwenye fikira zetu, Mungu amweke mahala pema peponi ''.
Bah alisifika sana kama mmojawapo wa wachezaji bora wa timu ya taifa la Sierra Leone hasa katika miaka ya 2000 hadi 2008.
Katika ngazi ya klabu , aliichezea timu ya ubelgiji ya KSC Lokoren hapo 1994-96 kabla ya kuelekea Korea kusini kuichezea Chunnam Dragons hapo 1997.
Miaka miwili baadae alielekea UChina na kuwa raia wa kwanza wa Sierra Leone kucheza katika ligi kuu itwayo Chinese Super league, akiwa katika klabu ya Xiamen Lanshi mwaka wa 1999-2003 kisha akahamia klabu ya Zhejiang Lucheng hapo 2004.
Pia aliwahi kuchezea klabu ya Halmstad BK huko Sweden.
ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG YETU WATARIFU NA WENZAKO PIA TUPIA MAONI YAKO

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles