» »Unlabelled » BIASHARA YA INTERNET JE UNAFAHAMU SIM YAKO NIMTAJI?

Kufanya Biashara katika Intaneti: Biashara 5 za Kuanza Nazo Bure
       UKIFA MASKINI NIUCHAGUZI WAKO MWENYEWE







Wajasiriamali wengi wamekuwa wakitafuta mbinu mbalimbali za kufanya biashara aidha kwa kuuza huduma au bidhaa. Lakini wachache sana hasa Afrika ambao wanafikiria kufanya biashara katika intaneti. Kuna mbinu nyingi tofauti za kufanya biashara katika intaneti ambazo zinatoa fursa kwa wajasiriamali kujiongezea kipato.
Kinachohitajika ni simu au kompyuta yenye kuunganishwa na mtandao wa intaneti na pia kuwa umejiunga na mitandao ya kijamii ,au mmiliki wa tovuti au blogu (ambazo unaweza kupata bure) au barua pepe.
Zifuatazo ni baadhi ya programu zinazokuwezesha kupata fedha kupitia intaneti:
1. Kuuza Bidhaa Za Biashara Yako Kupitia Tovuti 
Unaonesha biadhaa zako na bei,wanunuaji wanaziona na kuweka oda ya manunuzi. Wanalipa kwa Kadi ya Benki Credit /Debit Card) na fedha inaingia katika akaunti yako benki. Au kwa kutumia malipo kwa mfumo wa simu kama M-Pesa ,Tigo Pesa na Airtel Money kwa Tanzania.
2. Kuuza Bidhaa Za Biashara Ya Watu Wengine Kupitia Tovuti
Unajisajili na baadhi ya makampuni yanayouza bidhaa mtandaoni duniani kama Amazon na eBay na kisha kuonesha bidhaa zao katika tovuti au blogu au katika mitandao ya kijamii kama facebook na twitter. kisha watu wakinunua bidhaa hizi kupitia matangazo yako basi unapata kiasi cha malipo waliyofanya yaani kamisheni.
Kujiunga fuata linki:
§  eBay
 3. Kuuza Matangazo Kupitia Tovuti Au Blogu
Kuna makampuni mbalimbali dunia ambayo yana wakutanisha watangazaji na wauzaji kupitia matangazo katika tovuti au blogu.
Watangazaji wanajiunga nakutuma matangazo ya biashara yao na wauzaji wenye tovuti wanajiunga nakuruhusu matangazo kuonekana katika tovuti zao.
Wauzaji wa matangazo wanalipwa kila tangazo linapoonekana katika tovuti au watu wanapo bonyeza matangazo haya.
Mfano ni adsense , chitika , BuySellAds nk.
Unahitaji kuwa na tovuti au blog ili kufanikiwa katika programu hii.
4. Kufanya Kazi Za Ajira Kupitia Mtandao
Kuna makampuni ambayo yanataka wafanyakazi katika mtandao ambao wanaweza kufanya kazi fulani na wanalipwa wakikamilisha.
Baadhi ya kazi ni kama kutengeneza tovuti, kutengeneza programu za komputa au simu, kuchapa,kusikiliza na kutohoa suuti kwenda maandishi n.k
Badhi ya mitandao inyotoa huduma hizi ni  surveycompare.net , odesk.com,onlinejobs.net ,elance.com , peopleperhour.com na  fiverr.com

5. Kutangaza Biashara Kwa Kutuma Linki
Mbinu hii ndiyo hasa ninayopenda kuisisitiza hapa. Sababu ya kusisitiza nimkwasababu inafanya kazi kwa haraka na urahisi. Huhitaji kuwa na tovuti wala blogu kufanikisha. Kama tu upo katika mitandao ya kijamii kama facebook,twitter,intagram na mingine kama skype,whatsapp na pia kwa email unaweza kufanikiwa sana kwa kutuma linki ambayo marafiki zako wakiifungua utapata malipo.
Mfano Nimesoma katika intaneti kitu kizuri juu ya kupunguza unene na nataka marafiki zangu wanene wafidike kama haupo katika bishara hii nitatuma linki katika kundi katika facebook mfano na sitapata chochote.
Lakini ukiwa katika programu hizi unawezeshwa wewe kupata malipo kila unapofanya hivyo. Rahisi
Kama una marafiki wengi basi uwezo wako wa kufanikiwa ni mkubwa sana
Ifuatayo ni mitandao inayotoa huduma hii:



a

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...