» » Rais Magufuli Atangaza Ajira 3000 za Wanajeshi

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa nchi Dkt. John Pombe Magufuli, ametangaza kutoa ajira kwa wanajeshi 3000 wapya mwaka huu, ili jeshi la Tanzania liweze kuwa na askari wa kutosha.

Rais Magufuli ametoa taarifa hiyo leo alipokuwa akihutubia umma mara baada ya kuwapa kamisheni maafisa wa Jeshi, katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha, huku akitaka wahusika kutowasahau vijana waliohitimu mafunzo ya JKT.

"Lakini pia leo tumepata maofisa 422, unapokuwa na jeshi la maofisa lazima kuwepo na 'junior officers', huwezi ukawa na jeshi lote lina maofisa, kwa kutambua hili natangaza rasmi kwamba nitatoa nafasi 3,000 za kuajiri wanajeshi wapya, na hawa wataoajiriwa muzingatie na wale ambao wamemaliza JKT, lengo ni kuhakikisha jeshi letu linakuwa na maaskari wa kutosha na la kisasa zaidi", amesema Rais Magufuli.

Leo Rais Magufuli ametoa kamisheni kwa Maafisa wa Jeshi 422 waliohitimu mafunzo katika chuo cha Monduli, hafla ambayo imekuwa ya kwanza kufanyika katika uwanja wa umma,

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...