» » Mwili wa mtoto waokotwa mferejini Arusha

Mwili wa mtoto ambaye anakadiriwa kuwa na umri wa siku moja umeokotwa kwenye mfereji wa kupitisha maji machafu katika eneo la Mtaa wa Ali Nyanya kata ya Ungalimited jijini Arusha.

Kichanga hicho kimeonekana kutekelezwa na mama yake mzazi mara tu baada ya kujifungua na kupelekea kupoteza maisha, baadhi ya wananchi wa eneo hilo wamelaani kitendo hicho cha kinyama na kikatili kinachofanywa na baadhi ya wanawake wasiokuwa na hofu ya Mungu ndani yao ambao wanakatisha uhai wa watoto hao ambao hawana hatia.

Mwenyekiti wa Mtaa huo Omari Shehe naye amelaani kitendo hicho na kuahidi kushirikiana na vyombo vya dola kuhakikisha wanamtafuta muhisika ambaye amefanya tukio hilo la kinyama ili iwe fundisho kwa watu wengine wenye tabia hizo za kufanya uovu na ukatili huo.

Vitendo vya watu kutekeleza watoto vimekuwa vikishamiri katika maeneo mbalimbali ya nchi huku wengi wakionekana kufanya ukatili huo kutokana na baadhi ya wanaume kukataa watoto au ujazito jambo ambalo hata hivyo halikubaliki.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...