» » MC Pilipili amepata ajali na Kulazwa Bugando

Mchekeshaji maarufu nchini, Emmanuel Mathias maarufu Mc Pilipili amepokewa katika kitengo cha dharura cha Hospitali ya Rufaa Bugando, Mwanza baada ya kupata ajali mkoani Shinyanga.

Ofisa uhusiano wa hospitali hiyo, Lucy Joseph amethibitisha kupokewa Mc Pilipili na amesema taarifa zaidi kuhusu hali yake zitatolewa baadaye.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Simon Haule akizungumzia ajali hiyo, amesema Mc Pilipili alikuwa akimkwepa mwendesha baiskeli katika Kijiji cha Bubiki, Kata ya Mondo mkoani humo.

Amesema mchekeshaji huyo alikuwa akiendesha gari lililopata ajali akiwa na abiria mmoja ambaye naye amepata majeraha.

Katibu Muhtasi wa Kampuni ya Pilipili Events, Stella Maswenga amesema wamepokea taarifa za ajali hiyo jana Jumanne jioni.

“Bado tunahangaika, nafikiri wamepoteza kila kitu kwa maana simu zao hazipo hewani, pia hatuna taarifa zozote kuhusu wao zaidi ya kuambiwa wamewahishwa Bugando,” amesema.

Maswenga amesema Mc Pilipili alialikwa mkoani Shinyanga kwa ajili ya kusherehesha harusi wikiendi iliyopita na alikuwa akisafiri kuelekea Mwanza.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...