» » Mwalimu Afikishwa Mahakamani Kwa Kumbaka Mwanafunzi na Kumjaza Mimba

Mwalimu wa shule ya msingi katika kata ya Ligunga tarafa ya Matemanga wilaya Tunduru mkoani Ruvuma Rajabu Morisi amefikishwa katika Mahakama ya wilaya hiyo kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wake na kumsababishia ujauzito.

Akisoma shauri hilo no 148/2017, mbele ya mlinzi wa amani hakimu wa Mahakama ya mwanzo Itika Korosho, mwendesha mashtaka wa Mahakama ya wilaya Inspekta Bosco Kilumbe amesema mtuhumiwa alitenda kosa hilo kati ya mwezi January na Mei mwaka huu katika muda usiojulikana baada ya kumrubuni mwanafunzi huyo.

Na kudai kufanya hivyo ni kinyume cha sheria namba 130 (1) na (2e) na namba 131 (1) na (2) vya sheria ya kanuni ya adhabu sura namba 16 kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Hata hivyo mtuhumiwa huyo amekana kosa hilo upelelezi bado unaendelea , mtuhumiwa yupo nje kwa dhamana, kesi hiyo itatajwa tena Mahakamani Agosti 28 mwaka huu.

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles