» » Jeshi la Polisi Dar lakamata vifaa mbalimbali vya magari na Wezi 73

Jeshi la Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, limewakamata watuhumiwa 73 wa wizi wa magari pamoja na vifaa vya magari katika oparesheni yake maalum inayolenga kuwakamata wezi na wanunuzi wa vifaa vya magari.

Taarifa ya jeshi hilo, iliyotolewa jana na Kaimu kamanda wa Polisi kanda maalum Dar es Salaam, (DCP) L. J Mkondya inaeleza kuwa tarehe 21/07/2017 walifanikiwa kuwakamata wezi wa vifaa mbalimbali vya magari, ikiwa ni pamoja na wanunuzi wa vifaa hivyo katika sehemu mbalimbali za jiji la Dar es Salaam.

Katika Operesheni hiyo jumla ya watuhumiwa 73 wamekamatwa baada ya kupekuliwa walikutwa na vifaa mbalimbali vya magari ikiwemo, Side mirrors, taa za gari, bampas, left pump, milango ya magari, vitasa vya magari, power windows, radio, injector pump, starer na seat cover.

Watuhumiwa waliokamatwa katika mkoa wa kipolisi Kinondoni ni 29, Ilala 33 na Mkoa wa kipolisi Temeke ni 11, watuhumiwa hao walishindwa kuvitolea maelezo vifaa hivyo, na kuwa upelelezi bado unaendelea ili kubaini mtandao unaojihusisha na wizi huo ambapo watafikishwa mahakami mara tuu uchunguzi utakapo kamilika.

Kwa ujumla vifaa vyote vilivyo kamatwa ni, Radio 12, Taa za magari aina mbalimbali 105, side mirrors 92, vitasa vya gari 109, switch 7, Bampa 4, Left Pump 3, Air Cleaner 1, Booster 3, Show grill, Mashine ya kupandishia vioo 1 na Tyre used 2.

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...