» » Watu 30 wahukumiwa kifo Misri kwa mauaji ya mwendesha mashtaka

A picture taken on July 10, 2013 shows Egyptian state prosecutor Hisham Barakat sitting at his office in Cairo.

Haki miliki ya pichaSTR/AFP/GETTY IMAGES
Image captionHisham Barakat aliuawawa kwenye mlipuko
Mahakama ya Misri imependekeza adhabu ya kifo kwa watu thelathini waliotiwa hatiani kwa kuhusika kwenye mauaji ya mwendesha mashtaka mkuu wa nchi hiyo.
Hisham Barakat alikufa kwenye shambulio la bomu lililotegwa kwenye gari miaka miwili iliyopita.
Alikuwa miongoni mwa maafisa waandamizi wakuu kuuawa na wanamgambo katika miaka ya karibuni.
Bwana Barakati alihusishwa na maelfu ya kesi ya wapiganaji wa Kiislamu kufuatia mapinduzi ya serikali ya Misri iliyokuwa ikiongozwa na Muslim Brotherhood.
Mamlaka za dini za nchi hiyo sasa wataamua iwapo waidhinishe hukumu ya vifo iliyopitishwa na mahakama.
Egyptian security forces stand guard at the site of a bomb attack that targeted the convoy of Egyptian state prosecutor, Hisham Barakat, who died hours after the powerful explosion hit his convoy, in the capital Cairo on June 29, 2015.Haki miliki ya pichaKHALED DESOUKI/AFP/GETTY IMAGES
Image captionEneo la mlipuko mwaka 2015
Misri iliwalaumu kundi la Musclim Brotherhood na lile la Gaza la Hamas kwa mauaji ya Bwana Barakat licha ya makundi yote mawili kukana kuhusika
Mwaka uliopita wizara ya mambo ya ndani ilitoa video ikionyesha wanaume kadha wakikiri kuhusika kwenye mauaji hayo na kusema kuwa walienda huko Gaza kupata mafunzo kutoka kundi la Hamas.
Baadaye baadhi yao walikana madai hayo mahakamani wakisema kuwa walikuwa wameteswa ili kukiri.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS


tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...