» » Wanasayansi wavumbua chanjo ya magonjwa ya moyo

Netherland

Image captionMfano wa chanjo hiyo
Shirika la utafiti wa kisayansi kutoka nchini Netherlands limeanza kufanya majaribio kwa wanadamu ya chanjo ya kupunguza kiwango cha mafuta katika mwili wa mwanaadamu na kwamba endapo utafiti huo utafanikiwa; wana matumaini kuwa chanjo hiyo itakuwa na uwezo wa kuzuia magonjwa ya moyo.
Watafiti hao wameeleza kuwa majaribio yao waliyokwisha kuyafanya dhidi ya panya yanaonesha kwamba chanjo hiyo imefanikiwa kuzuia na kuacha kuimarisha amana ya mafuta katika mishipa ya damu.
Imearifiwa kuwa chanjo hiyo ina uwezo wa kufanya mfumo wa kinga ya mwili kukabiliana na mafuta yasiyohitajika kutoka katika damu.
chanjo
Image captionJe watu wenye miili mikubwa wamepata ukombozi?
Wanasayansi hao wanaamini kuwa chanjo hiyo inaweza kutumika kama njia mbadala wa zilizokuwa za kupunguza mafuta , pamoja na kuwasaidia, mamilioni ya watu ulimwenguni kupambana na mafuta yasiyohitajika mwilini.
Inatarajiwa kuchukua takriban miaka sita ili vipimo hivyo kukamilika.


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...