» » Marekani yaitaka China kuikanya Korea Kaskazini


Waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Rex Tillerson

Image captionWaziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Rex Tillerson
Marekani imeishinikiza China kuongeza jitihada zake katika kuizuia Korea Kaskazini kuendelea na mipango yake ya kinyuklia pamoja na utengezaji wa makombora.
Akizungumza baada ya kukutana na maafisa wakuu wa China, waziri wa maswala ya kigeni nchini Marekani Rex Tillerson amesema kuwa Beijing ina jukumu la kidiplomasia kuongeza shinikizo zaidi kwa Pyongyang iwapo ingetaka kupunguza wasiwasi katika eneo hilo.
Katika mkutano huo mjini Washington ambao ulihudhuriwa na waziri wa Ulinzi wa Marekani James Mattis bwana Tillerson alisema kuwa China inaunga mkono mpango wa Marekani wa kusitisha mpango wa kinyuklia wa Korea Kaskazini pamoja na majaribio ya makombora ya masafa marefu.
Pia ameyataka mataifa yote kuongeza juhudi za kumaliza biashara ya kihalifu ya Korea Kaskazini ambayo anasema inatumika kufadhili mipango yake ya Kinyuklia.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440


tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn news

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles