» » Jumba la ghorofa saba laporomoka Nairobi Kenya

Jumba la ghorofa saba laporomoka Nairobi

Image captionJumba la ghorofa saba laporomoka Nairobi
Karibu watu 15 hawajulikani waliko baada ya jumba la ghorofa saba kuporomoka usiku wa kuamkia Jumanne, katika kitongoji kimoja cha mji mkuu wa Kenya, Nairobi.
Shirika la msalaba mwekundu nchini Kenya, liliandika kwenye mtandao wa twitter kuwa makundi ya uokoaji yako eneo la mkasa katika kijiji cha Kware Pipeline mtaa wa Embakasi.
Gazeti la Star nchini Kenya lilisema kuwa watu kadha waliokolewa kabla ya jumba hilo kuporomoka.
Jumba la ghorofa saba laporomoka Nairobi
Image captionJumba la ghorofa saba laporomoka Nairobi
Walioshuhudia waliliambia gazeti hilo kuwa jumba hilo lilikuwa limeonyesha dalili baada ya nyufa kuonekana kwenye kuta zake.
Mratibu wa shughuli za uokoaji Pius Masai anasema kuwa zaidi ya watu 100 wanatambulia kuwa salama lakini akaongeza kuwa huenda watu wengi wamekwama.
Idara inayoshughulikia majanga inasema kuwa familia nyingi ziliondoka wakati ziliamriihwa kabla ya jengo hilo halijaporomoka ambapo watu 121 waliondoka salama.
Jumba la ghorofa saba laporomoka Nairobi
Image captionJumba la ghorofa saba laporomoka Nairobi
Vyombo vya habari vinasema kuwa baadhi ya watu walirudi tena ndani jengo hilo kuchukua mali yao wakatai liliporomoka.
Polisi wanasema kuwa hawafahamu ni watu wangapi ambao wamekwama ndani ya jengo lililopomoka.
Jumla ya watu 49 walifariki wakati jumba lingine liliporomoka kufuatia mvua kubwa mwezi Aprili mwaka huu.
Jumba la ghorofa saba laporomoka Nairobi
Image captionJumba la ghorofa saba laporomoka Nairobi

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440



BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS



tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...