» » Imeanza tena: Korea Kaskazini yarusha kombora la kushambulia meli

Korea Kaskazini ikionyesha makombora ya Styx 2012

Haki miliki ya pichaAFP/GETTY IMAGES
Image captionKorea Kaskazini ikionyesha makombora ya Styx 2012
Korea kaskazini imerusha makombora kadha ya kushambulia meli mashaiki mwa pwani yake, kwa mujibu wa Korea Kusini
Mamlaka zilisema kwa makombora hayo yaliyorushwa Alhamisi asubuhi karibu na mji wa Wonsan yalikuwa ni ya masafa mafupi.
Makombora hayo yaliruka umbali wa kilomita 200 kabla ya kuanguka baharini.
Majaribio ya makombora ya Korea Kaskazini mwaka huu yamekiuka vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
Wataalamu wana hofu kuwa majaribio hayo na hatua za Korea kutundika silaha za nuklia katika vichwa vya makombora.
Map of North Korea showing Wonsan in east
Image captionRamani ya Korea Kaskazini
Msemaji wa Jeshi la Korea Kusini amesema kuw majiribio ya hivi punde yalionyesha kuwa Korea Kaskazini ilitaka kuonyesha kuwa ina uwezo wa kulenga meli kubwa baada ya mazoezi ya hivi majuzi kati ya Marekani na vikosi vya Korea Kusini.
Makomboa ya kushambulia meli ni makombora ambayo huelekezwa. Mwaka 2012 Korea Kaskazini ilionyesha makomboa kadha kama hayo yanayojulikana kama Styx.
Lakini hapo awali Korea ilijaribu bila mafanikio kufanyia majaribio makombora ya kushambulia meli.
Marekani inaweka mitambo ya kujikinga nchini Korea KusiniHaki miliki ya pichaEPA
Image captionMarekani inaweka mitambo ya kujikinga nchini Korea Kusini


Tuma picha/ habari what-sap 0769436440



BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS



tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles