» » Trump atabiri mazungumzo na Xi yatakuwa ‘Mazuri,’ ‘Magumu’

Trump atabiri mazungumzo na Xi yatakuwa ‘Mazuri,’ ‘Magumu’


Rais Donald Trump- Rais Xi Jinping
Rais Donald Trump- Rais Xi Jinping
Rais Donald Trump anatarajiwa kumpokea Rais wa China Xi Jinping kuanzia Alhamisi katika Jumba lake la Mara-Lago lilioko ufukweni katika eneo la Kusini ya Marekani.
Lakini inawezekana hali halisi isiwe ya uchangamfu kama ilivyo hali ya hewa ya Florida.
Trump ametuma kupitia Twitter utabiri wake kuhusu mkutano wake wa kwanza na Rais wa China, akisema utakuwa na mazungumzo “magumu sana,” kwani Marekani “haiwezi kukubali kubakia kuwa na upungufu wa kibiashara na uhaba wa ajira.”
Katika mkutano wake ikulu ya White House wiki iliopita, Trump aliwaambia wenye viwanda vilivyoko Marekani watakuja “kushangaa” watapomuona akiwa na Xi.
“Natarajia kwa hamu kubwa kukutana naye na ujumbe wake. Na tutaona kile kitakachotokea,”amesema Trump. Kiongozi huyo wa China sio rahisi kuja mikono mitupu.

“Nimatarajio yangu kuwa Wachina watamtuma Xi hapa akiwa na kitita cha zawadi kubwa nzuri na za ukarimu, katika masuala ya uwekezaji wa miundo mbinu ndani ya Marekani, na kumsaidia Rais Trump kuleta ajira ambazo alikuwa amewaahidi wapiga kura,” Mtafiti wa ngazi ya juu wa Stimson Center Yun Sun ameiambia VOA.
“Jambo la kijinga linaweza kutokea…’
Baadhi ya wanaofuatilia China wametahadharisha kuwa sio kila kitu kitaenda vile kilivyopangwa, kwani jambo hili ni mapema sana kwa uongozi wa Trump kwani mengi bado hayajaorodheshwa.
“Kitu cha kijinga kinaweza kutokea bila ya kutarajia, bila shaka. Unajua ujumbe mmoja wa Tweet unaweza kubadilisha muelekeo wa mkutano kwa kiwango fulani,” amesema naibu mkurugenzi wa tafiti za China (CSIS), Scott Kennedy.
“Lakini ninategemea kutakuwa na lawama bila ya kuwa hasa na mazungumzo mengi, na baadae Wachina wataondoka wakiwa na wasiwasi.”
Tuma picha/ habari what-sap 0769436440



BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS
https://play.google.com/store/apps/details?id=com.sn.news&hl=en



tupe maoni yako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles