» » Magari yasiyo na dereva kuanza kutumika London

Magari yasiyo na dereva kuanza kutumika London

Haki miliki ya pichaOXBOTICAImage captionMagari yasiyo na dereva kuanza kutumika London

Wasafiri katika mji mkuu wa Uingereza London, hivi karibuni wataanza kutumia magari ya usafiri yasiyo na dereva.

Katika kipindi cha majuma matatu yanayokuja karibu watu 100 wataanza kutumia magari hayo katika eneo la Greenwwich mjini London.,

Magari hayo ambayo husafiri kwa hadi kasi ya kilomia 16.1 kwa saa, yataelekezwa na kompyuta.

Uber yaondoa magari yanayojiendesha barabaraniApple kuunda magari yanayojiendesha

Hata hivyo kutakuwa na mtu ndani ya gari hilo ambaye anaweze kulisimamisha ikiwa itahitajika.

Haki miliki ya pichaGATEWAYImage captionMagari yasiyo na dereva kuanza kutumika London

Oxbotica, ambayo ni kampuni iliyounda magari hayo, ilisema kuwa watu 5000 wametuma maombi ya kutaka kushiriki katika majaribio hayo.

Magari hayo yanawabeba watu wanne na hayana usukani wala breki

Uber teksi kuzindua magari yanayojiendeshaGari la umeme lampeleka mmiliki hospitalini

Gari hilo lina kamera ambayo inaweza kuona umbali wa mita 100 na husimama wakati kuna kitu chochote mbele yake.

Maafisa wa mradi huo wanaamini kuwa magari hayo, yatasaidia katika kuboresha usafiri eneo la Greenwish jijini London.

Mshirikishe mwenzako

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles