» » Kinara wa upinzani nchini Zambia azuia msafara wa Rais

Kinara wa upinzani nchini Zambia azuia msafara wa Rais

Image captionBw Hakainde Hichilema, ni kiongozi mkuu wa upinzani nchini Zambia

Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Zambia Hakainde Hichilema, alizuia msafara wa Rais wa nchi hiyo Edgar Lungu mwishoni mwa juma.

Hii ni kulingana na taarifa iliyotolewa kutoka kwa msemaji wa rais.

Upinzani unaongoza kwa kura za urais ZambiaKinara wa upinzani nchini Zambia azuia msafara wa RaisWaliofanya ghasia wakamatwa Zambia

Amos Chanda, amesema kuwa msafara wa Bw Hichilema, iliendelea kudumisha njia yake ya kupitia magari barabarani, badala ya kuondoka barabarani ili kupisha msafara wa magari ya Rais kuweza kupita.

Haijafahamika iwapo hatua hiyo inatokana na kisa cha mara kwa mara cha kuvamia nyumba ya Bw Hichilema iliyoko katika mji mkuu, Lusaka.

Kwa sasa kiongozi huyo anazuiliwa katika kituo cha polisi.

Ameliambia gazeti moja la Afrika Kusini- Daily Maverick kwamba, rais anataka kumuuwa.

Bw Hichilema, alipewa dhamana mwezi Oktoba mwaka jana, baada ya kushtakiwa kwa kosa la fitna, hatua ambayo kikosi chake kilisema ni mbinu za chama tawala za kutaka kumnyamazisha.

Mshirikishe mwenzako 

Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About IVST TANZANIA

Hi my name is Gasto Alex Didas
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...

Popular Articles