» » Bungeni: Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama Kukutana Leo Kujadili Mauaji ya Polisi 8 na Raia

Bungeni: Kamati ya Bunge ya Ulinzi na Usalama Kukutana Leo Kujadili Mauaji ya Polisi 8 na Raia

Mbunge wa Bukombe, Mhe. Dotto Biteko ametoa hoja ya kuahirishwa kwa shughuli za bunge ili Bunge liweze kujadili hali ya mauaji inayoendelea nchini ikiwemo mauaji ya askari polisi waliouawa na watu wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi katika eneo la Jaribu Mpakani, Wilaya ya Kibiti Mkoani Pwani. 

Hoja hiyo imeungwa mkono na wabunge kadhaa wakiwemo Cosato Chumi (Mafinga Mjini) na Amina Mollel (Viti Maalum)

Akitolea ufafanuzi hoja hiyo Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe Mwigulu Nchemba amesema serikali inachukulia jambo hilo kwa ukubwa na uzito mkubwa.
 
“Kama ilivyotolewa kauli na Waziri Mkuu serikali inalichukulia mambo haya kwa uzito mkubwa na inawahakikishia wananchi matukio ya uhalifu yaliyotokea ndio yametupa chachu zaidi ya kupambana na matukio kama haya na pia tunawaomba wananchi watoe taarifa na wala wasiogope maana tuna mfumo bora sana wa kuwalinda watoa taarifa wote” Ameeleza Waziri Nchemba ambaye pia ametoa pole kwa familia za askari wote waliopoteza maisha wakiwa katika kazi ya kulinda wananchi na amani ya nchi.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Job Ndugai, amelieleza Bunge kwa kuwa Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama chini ya Mwenyekiti wake Balozi Adad Rajabu itakutana leo na mawaziri husika ili kupokea taarifa ya mambo haya ni vyema Bunge likatoa nafasi kwa kamati hiyo kukutana kwanza na kupokea taarifa hiyo.

Tuma picha/ habari what-sap 0769436440

BONYEZA HAPA KUPATA APP YA 4SN NEWS

tupe maoni yako

Pakua App Yetu-Bofya Hapa Flower
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI

About 4sn News

Hi my name is Gasto Alex Didas from Mwanza Tanzania I'm blog manager and I have an App which is called 4sn News, my office is located in Rock City Mwanza-Tanzania at Miembeni "B" Street. My contacts +255769436440/ +255659750504 Welcome.
«
Next
Newer Post
»
Previous
Older Post

No comments:

Popular Articles

MBUNGE MABULA AKAGUA SHULE NNE MPYA ZA MSINGI, ZENYE THAMANI YA TSH 1.174 BIL, ASHAURI HALMASHARI KUTUMIA MCHORO MPYA WA TAMISEMI KUOKOA MADARASA 3 KILA SHULE

Mhe. Stanslaus Mabula Mbunge Jimbo La Nyamagana amefanya ziara ya kikazi katika Kata nne za halmashauri ...